Wednesday, November 21, 2018

RC HAPI AWASHA UMEME MAFINGA NA KUIPONGEZA TANESCO


Na Amani Mbwaga, Mafinga.

Mkuu wa Mkoa Iringa Mhe Ally Salum Hapi leo amepata fursa ya kutembelea na Kuwasha mradi wa umeme wa REA awamu ya III Mzunguko wa Kwanza katika mtaa wa Ndolezi ulipo Halmashauri ya Mji Mafinga wilaya ya Mufindi, Mkoani Iringa 


Mradi huo ulioanza kutekelezwa tarehe 3 Julai 2017 na kampuni ya M/S Sengerema Engineering Group Ltd wenye gharama ya jumla ya Tsh Bilioni 24.7 chini ya Usimamizi wa Shirika la Umeme Tanzania TANESCO.

“Umeme ni nyenzo muhimu sana kwa wananchi wetu hasa vijijini, Serikalli ya awamu ya tano inayoongozwa na Rais Dkt John Pombe Magufuli kupitia ilani ya chama acha mapinduzi tumedhamiria kuhakikisha vijiji vyote kwenye nchi yetu vinapata umeme wa uhakika” alisema Mhe Hapi.

Aidha Mhe Hapi ameamua mwenyewe kuanza kufuatilia miradi ya REA ili kujiridhisha kama kasi ya upelekaji umeme vijijini inaridhisha na alisema “Nataka niwahakikishie kuwa hakuna kijiji hata kimoja kwenye mkoa wetu ambacho kitabaki bila kupata umeme hiyo ni ahadi ya Mhe Rais na mimi kama muu wenu wa mkoa tutaendeleakufuatilia kuhakikisha wananchi wetu wote wanapata umeme katika vijiji vyote.”

Mhe. Hapi amesisitiza kuhakikisha umeme unapokwenda vijijini ni lazima kutoa kipaumbele cha ugawaji wa umeme katika maeneo muhimu kwanza ya zahanati, visima vya maji, na shuleni.

Jumla ya wateja 2596 wanategemewa kuunganishwa na umeme kati yao 2333 ni wa njia moja na 263 ni wa njia tatu na mpaka kufikia tarehe ya leo jumla ya vijiji 18 vimeungwa umeme na Transfoma 18 zimefungwa katika maeneo mbalimbali ya mradi.

Mkuu wa Wilaya Mufindi Mhe Jamhuri William akitoa salamu za wilaya kwa mkuu wa mkoa alisema kupitia mradi wa umeme vijijini REA,  Wananchi wa Ndolezi walikua na shida sana ya umeme na walipiga kelele sana lakini aliwambia umeme utafika tu na sasa uefika.

Kwa kupitia juhudi za Mbunge wa Mafinga mjini Mhe Cosato Chumi alipiga kelele sana bungeni lakini aliwasumbua sana TANESCO na hatimae leo umeme umewashwa rasm” alisema Mhe. William.

Kwa Upande wake Mwenyekiti wa bodi ya Shirika la umeme Tanzania TANESCO Profesa Alexander Kyaruzi ameipongeza serikali ya awamu ya tano inayoongozwa na Rais Dkt John Pombe Magufuli kwani amedhamiria kulitoa Taifa hili kwenye hali lilipo na kulipeleka kwenye uchumi wa kati ambao utaendana na Tanzania ya viwanda.

Lakini huwezi kwenda katika uchumu wa kati wakati watu wako gizani, kwa hiyo rais ametoa fedha nyingi sana kupitia REA ili kupata umeme wa uhakika vijijini.

“Iringa kwa awamu hii takribani vijiji 179 vitapata umeme na ikija awamu ya III Mzunguko wa pili kila Mtanzania atapata umeme na hili Mhe Rais amedhamiria haswaa ifikapo 2021 kila Mtanzania awe na umeme na kwa mujibu wa takwimu zilizopo kwa sasa asilimia takribani 67.5 umeme umewafikia wananchi kote nchini” alisema Profesa Kyaruzi.

Akisoma taarifa ya utekelezaji wa mradi wa umeme kwa Mkuu wa Mkoa Iringa Meneja TANESCO Wilaya ya Mufindi Mhandisi Omary Ally amesema Jumla ya wateja 616 wamelipia kuunganishiwa umeme kati yao 263 wameunganishwa na 353 bado hawajaunganishwa kutokana na ukosefu wa Mita kutoka kwa mkandarasi.

Aidha kwa mujibu wa Mkandarasi wa REA Kampuni ya M/S Sengerema Engineering Group Ltd inyotekeleza mradi huu kupitia kwa Mhandisi Bryson Chegula amemthibitishia Mkuu wa Mkoa na wananchi wa Ndolezi na Mafinga kwa ujumla kuwa zaidi ya Mita  1000 za umeme zinainga siku ya Jumapili hali itakayochochea uunganishwaji wa wateja wengi wa umeme na hatimae kuondokana na changamoto yakukosa umeme. 

“Wilaya ina jumla ya vijiji/mitaa 161 na vitongoji 562 kati ya hivyo vijiji/mitaa 95 vimeshapata umeme REA I&II na vijiji 54 vipo kwenye REA awamu ya III Mzunguko wa kwanza katika utekelezaji” alisema Mhandisi Omary.

Kukamilika kwa miradi ya umeme awamu ya kwanza, ya pili na ya tatu itachochea kwa kiasi kikubwa maendeleo ya viwanda vidogo vijijini na kuongeza wigo mkubwa kwa wananchi wa Mufindi waliofikiwa na huduma ya umeme hatimae kukua kwa uchumi na hatimae kuongeza pato la Taifa.


HABARI PICHA
Mkuu wa Mkoa Iringa Mhe Ally Hapi akikata utepe kuashiria kuwasha umeme rasmi katika Mtaa wa Ndolezi Mjini Mafinga, Kushoto kwake ni Mwenyekiti wa Bodi ya TANESCO Profesa Alexander Kyaruzi, anaefuatia ni Mkuu wa Wilaya Mufindi Mhe Jamhuri William na kulia kwa Mkuu wa mkoa ni Mwenyekiti wa Halmashauri yaMji Mafinga Mhe Charles Makoga
Mkuu wa Mkoa Iringa Mhe Ally Hapi akiongea na wananchi wa mtaa wa Ndolezi kabla ya kuwasha umeme

Mkuu wa Wilaya Mufindi Mhe Jamhuri Davidi William akitoa salamu za Wilaya
Mwenyekiti wa Halmashauri ya Mji Mafinga Mhe Charles Makoga akitoa neno la Shukrani

Mwenyekiti wa Bodi ya Shirika la Umeme Tanzania Profesa Alexander Kyaruzi akitoa salamu za TANESCO Makao Makuu
Meneja wa TANESCO Wilaya ya Mufindi Mhandisi Omary Ally akitoa taarifa ya utekelezaji wa mradi wa Umeme kwa Mkuu wa Mkoa wa Iringa Mhe Ally Saul Hapi
Wananchi wa Mtaa wa Ndolezi Mjini Mafinga Wakifurahia kuwashwa kwa umeme katika mtaa wao na kuipongeza serikal kupitia TANESCO kwa kuwafikishia huduma hiyo muhimu kwa maendeleo ya Uchumi wa Taifa





Mkuu wa Mkoa Iringa Mhe Hapi akisalimiana na Mwenyekiti wa Bodi ya Shirika la Umeme Tanzania Prof. Kyaruzi

 


Baadhi ya watumishi wa serikali ikiwemo kamati ya ulinzi na usalama wilaya ya mufindi wakifuatilia kwa karibu zoezi la uwashwaji wa umeme katika mtaa wa Ndolezi Mjini Mafinga









Mkuu waMkoa Iringa Mhe Hapi Akiongea na Wananchi wa Mtaa wa Ndolezi


Mkuu wa Mkoa Iringa  Mhe Hapi (Kulia ) akimkabidhi Kisemeo Meneja TANESCO Mufindi Mhandisi Omar Ally Kujibu hoja za wananchi mbalimbali kabla ya kuzindua uwashaji wa umeme katika mtaa wa Ndolezi.



Wananchi wa Mtaa wa Ndolezi wakimsikiiza kwa makini Meneja TANESCO Wilaya ya Mufindi Mhandisi  Omary Ally


Mmoja wa Wafanyakazi wa TANESCO akisubilia kwa hamu kuzinduliwa rasmi kwa uwashaji wa Umeme katika Mtaa wa Ndolezi



Mkuu wa Mkoa Iringa Mhe Hapi akipata ufafanuzi wa suala la Mita kutoka kwa Mkandarasi wa REA M/S Sengerema Engineering Group LTD  Mhandisi Bryson Chengula 


Mwakilishi wa Meneja TANESCO Mkoa wa Iringa (Kushoto) akitolea ufafanuzi wa baadhi ya mambo ambayo TANESCO Iringa inatarajia kuyakamilisha kabla ya 2021 ili kila Mtanzania na hususani Iringa awe na Umeme


Tayari kwa umeme Kuwashwa Rasmi Mtaa wa Ndolezi




Taa imewashwa rasmi na Mkuu wa Mkoa Iringa Mhe Hapi kuashiria uwashaji wa umeme Katika Mtaa wa Ndolezi




Mkuu wa Mkoa Iringa akiondoka eneo la tukio mara baada ya kukamilisha shughuli ya uwashaji wa umeme katika Mtaa wa Ndolezi Mafinga Mjini (Picha zote na Amani Mbwaga)

Kwa Maoni au Ushauri Wasiliana nasi;
Mob: +255 656 632 566
E-mail:prof.mbwaga@gmail.com
Twitter:@Amanimbwaga

No comments:

Post a Comment