Friday, December 21, 2018

Sao Hill Forest FC yawasili Jijini Dar es salaam tayari kwa Michezo ya Kirafiki na Kushinda Mechi ya Kwanza.


Na Amani Mbwaga, Dar es salaam.

Wakala wa Huduma za Misitu Tanzania (TFS) Shamba la Miti Sao Hill, kupitia timu yake ya mpira wa miguu imewasili vyema jijini Dar es salaam Jana usiku ikitokea Mafinga Wilayani   Mufindi Mkoani Iringa.

Kiongozi wa Msafara na Mwenyekiti wa Misitu Sports Bonanza ambae pia ni Afisa Nyuki wa Shamba la miti Sao hill Bwana Said Aboubakar amesema timu imewasili vyema na iko tayari kwa michezo mbalimbali ya kirafiki ambayo imeanza mapema leo hii ambapo iliikutanisha      Sao Hill Forest FC Vs Juhudi FC katika uwanja wa Kinesi muda wa saa 10:00 Jioni ambapo Sao Hill Forest imeibuka mshindi wa Magoli 02 kwa 0, Magoli yote yalifungwa na mchezaji mahiri Barnaba Mlomo Dk ya 19 na Dk 39.

Aidha kesho tarehe 22 Desemba 2018 saa 10:30 jioni mchezo wa kirafiki utaendele baina ya  KMC B Vs Sao hill Forest Fc katika Uwanja wa Shule ya Sheria (School Of Law) Dsm kuanzia saa 10:30 jioni.

Tarehe 23 Disemba 2018 saa 2 :00 asubuhi itakuwa ni Udsm FC Vs Sao Hill Forest  Fc Uwanja wa Taifa (Shamba la Bibi),  tarehe 24 Disemba 2018 saa 10:30 jioni ni Azam B Vs Sao Hill Forest FC Katika Uwanja wa Chamazi na Tarehe 25 Disemba 2018 ni Simba Sports Club B FC  Vs Sao Hill Forest FC uwanja wa Kinesi saa 2:00 Asubuhi.

Ziara hii ya kimichezo ni matokeo ya Michezo ya Misitu spots bonanza iliyozikutanisha timu takribani 32 kutoka katika zaidi ya vijiji 60 vinavyolizunguka shamba la miti Saohill ambapo miongoni mwao walichaguliwa takribani wachezaji 23 ambao wameunda timu ya misitu iliyoko chini ya wakala wa huduma za misitu Tanzania (TFS) Shamba la miti Sao Hill.

Aidha lengo kuu ni kurudisha shukrani kwa jamii inayozungukwa na shamba yaan (Corporate Social Responsibility) na kupitia michezo hii kunawasaidia vijana kujipatia ajira, kuvumbua vipaji vyao na kuviendeleza sanjari na kulitangaza shamba.

Shamba hili lilianzishwa mwaka 1939, na ndilo kubwa kati ya mashamba 23 ya taifa lina ukubwa wa hekta 135, 903 ambazo zimehifadhiwa kwa ajili ya upandaji miti na hifadhi ya mazingira, kati ya eneo hilo kiasi cha hekta 86,003 ni kwa ajili ya upandaji miti kibiashara, hekta 48,200 kwa ajili ya utunzaji  wa mazingira na vyanzo vya maji pamoja na ufugaji wa nyuki na hekta 1,700 ni kwa ajili ya makazi na uwekezaji, aidha shamba hili huchangia sana katika Pato la Taifa.

HABARI PICHA


Sao Hill Forest FC

Juhudi FC
Sao Hill Forest FC Wakiwa katika Picha ya Pamoja na Juhudi FC Katika mechi ya Kirafiki Uwanja wa Kinesi

Wachezaji wa akiba


Barnaba Mlomo

Emmanuel Ernest

Hashim Bakari
Frank Ndola



Godfrey
Pan Sanga



James Chogela

Jonhson Mkushi
Nesto Simon
Steven
Wilson Kangusi



Stanley Kadege

Daniel Kibiki (Kinyambe)
Robert Mgindo
Said Aboubakar



Casto Jerry

Merick Mbembe

Kocha Mkuu  Sao Hill Forest FC Bakari Khasim (Kushoto) akibadilishana machache na Kocha Msaidizi Khalid Nguchuke wakati wa mchezo wa kirafiki dhidi ya Juhudi FC katika Uwanja wa Kinesi Ubungo Dar es salaam.



Wachezaji wakifanya mazoezi (Warm Up)






Kocha Mkuu Sao Hill Forest Fc Bakari Khasim akitoa maelekezo kwa wachezaji












Baadhi ya washabiki wakifuatilia kwa makini mtanange mkali wa Juhudi FC Vs SaoHill Forest Fc Katika Uwanja wa Kinesi Ubungo Dsm (Picha zote na Amani Mbwaga)

Wednesday, December 19, 2018

Halmashauri ya Wilaya Mufindi Yatekeleza Kwa Vitendo Agizo la Waziri wa Mifugo na Uvuvi

Na Amani Mbwaga, Mufindi.
Baadhi ya Viongozi wa Majosho wakiwa katika picha na Kaimu Mkurugenzi
Halmashauri ya Wilaya ya Mufindi Imetekeleza agizo la Waziri wa Mifugo na uvuvi Mhe Luhaga Mpina aliloitoa Disemba 16 akiwa Wilayani Chato Mkoani Geita kuzindua kampeni ya Uogeshaji Mifugo ambapo aliziagiza Halmashauri kote nchini kutekeleza agizo hilo.

Agizo hilo ni kuhusu ugawaji wa dawa za ruzuku kutoka serikalini na kuogeshea mifugo bure kwa wafugaji wote ndani ya miezi 6 katika majasho kote nchini na Mufindi ikiwemo ambapo takribani maboksi 36 ambapo kila boksi lina makopo ya dawa 6 yenye lita 1 na lingine nusu lita Maboksi yamegawiwa bure yakiwa na  dawa aina ya Paranex ambapo inakadiriwa karibu majosho yote yanaujazo wa maji tkribani Lita 1200 hivyo dawa hizo zinatosha kwa josho moja.

Akigawa dawa hizo mgeni rasmi wa shughuli hiyo Kaimu Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya Mufindi Bwana Isaya Mbenje amewaasa wafugaji kufuga kisasa na kwa ubora unaotakiwa na ndio maana serikali imeamua kutoa ruzuku ya asilimia 100 kwa dawa hizo ili kusaidia wafugaji kuogesha mifugo yao.

“Dawa hii ikawe kichocheo kwa wafugaji kuogesha mifugo yao na baadae sisi kama wafugaji lazima tuone namna ya kuendeleza majosho yetu na ni lazima mhakikishe mifugo yenu inaogeshwa kwa ratiba kama mlivyojwekea, Ndugu zangu serikali inasisitiza kuogesha mifugo ili kupunguza gharama za kutibu mifugo hiyo na pale inapopatwa na magonjwa yatokanayo na kutoogeshwa”. Alisema Bwana Mbenje

Aidha ameagiza serikali za vijiji kuanza kutunga sheria ndogo za vijiji kuhusu uogeshaji kama kijiji hakina sheria ndogondogo basi watendaji wa vijiji wameagizwa kuhakikisha wanatunga sheria hizo za kumtaka kila mwenye mifugo analazimishwa kuogesha na kama hataki basi sheria kali zichukuliwe dhidi yake.

Kwa upande wake Mkuu wa Idara ya Mifugo na Uvuvi Halmashauri ya Wilaya Mufindi Bwana Elias Jamvia alisema kama walivyosikia katika vyombo vya habari mbalimbali kwamba serikali imetoa dawa ya ruzuku ya kuogesha mifugo kwa asilimia 100 nchi nzima ni pamoja na Halmashauri ya Wilaya Mufindi

Alibainisha kwamba idara yake inafanya kazi kwa kufuata miongozo, sheria na kanuni mfano leo hii wanasheria ndogo za Halmashauri zinazomtaka mtu asipoogesha wala kuchanja mifugo yake basi anatozwa faini ya shilingi 3000,000 au kifungo cha miezi 12 au vyote kwa pamoja.
“Wito wangu dawa hii iende ikafanye kazi iliyokusudiwa na serikali na si vinginevyo lakini pia majosho hayo yakawe endelevu Alisema Bwana Jamvia.

Kwa mujibu wa maelekezo toka Wizarani mfugaji ataogesha kwa muda wa miezi 6 bure lakini baada ya hapo ataanza kuchangia kidogo ili kupata fedha ya kununulia dawa ili majosho yawe endelevu.
Aidha Daktari wa Mifugo wa Halmashauri ya Wilaya Mufindi Bwana Robert Semaganga alisema kwa sasa Halmashari hiyo inakabiliwa na magonjwa ya kupe ukiacha yale ya kuambukiza kama vile homa ya mapafu na chambavu lakini pia kuna tatizo la minyoo.

Halmashauri kupitia idara ya Mifugo na uvuvi ina mpango mkakati wa kuhakikisha mifugo yote inachanjwa na kukomesha kabisa magonjwa hayo  lakini pia kuna ratiba za chanjo kwa mwaka mzima.

“Rais wetu ameamua kutoa dawa hizi bure mnaona jinsi gani serikali yetu inavyotujali sisi wafugaji hivyo dhamana yetu ni kutekeleza na kufanya yale ambayo waziri ametuagiza na amesema atatembelea majosho hayo kujionea utekelezaji wa agizo lake” alisema Bwana Semaganga.

Kwa mujibu wa Muongozo wa matumizi ya dawa za uogeshaji unawataka viongozi wa serikali ya kijii kusimamia sheria na kuwachukulia hatua wasiofuata, lakini pia kupokea na kutathimini taarifa ya uendeshaji wa josho kulingana na kanuni za katiba ya kikundi.

Kamati ya uendeshaji Majosho nayo ina kazi ya kuhamasisha wafugaji na kuhimiza uogeshaji, kuweka utaratibu wa kuendesha na kusimamia uogeshaji, kukusanya pesa zitokanazo na uogeshaji na kuziwasilisha benki na hatimae kutoa taarifa katika Idara ya Mifugo aidha Afisa ugani atakuwa msimamizi wa josho na kutoa ushauri kwa kamati.

Uzinduzi rasmi wa uogeshaji bure utazinduliwa hivi karibuni katika kata ya sadani na hafla hiyo ya ugawaji dawa bure ulihudhuriwa na Viongozi wote wa majosho 36 yaliyopo katika Halmahsuari ya Wilaya Mufindi wakimwemo wenyeviti, makatibu watunza hazina, wenyeviti wa vijiji na maafisa ugani wa kata zote.





HABARI PICHA


























Picha zote na Amani Mbwaga