Monday, May 28, 2018

Mapokezi ya Mwenge wa Uhuru 2018 yafana sana Halmashauri ya Mji Mafinga

 ·        Miradi ya Maendeleo yenye Thamani ya Zaidi ya Bilioni 1.7 Imezinduliwa, Kukaguliwa na Kuwekewa jiwe la Msingi.
Mkuu wa Wilaya Mufindi Mhe Jamhuri David William akipokea Mwenge wa Uhuru tayari kwa Kuukimbiza katika Halmashauri ya Mji Mafinga

Na Amani Mbwaga, Mafinga Iringa
 Jumla ya Miradi 08 imepitiwa na Mwenge wa Uhuru ikiwa ni utekelezaji wa miradi mbalimbali ya maendeleo katika Halmashauri ya Mji Mafinga, ikishirikiana na Wananchi pamoja na wadau mbalimbali wa Maendeleo.

Thamani ya miradi yote ni zaidi Tsh. Bilioni, 1.7, Mchanganuo wa gharama za miradi 08 ni kama ifuatavyo- ; Serikali Kuu imechangia Tsh Milioni 700.4, Halmashauri ya Mji Mafinga Tsh Milioni 47.2 Wahisani Tsh Milioni 38 na Wananchi wamechangia nguvu kazi na Fedha taslimu zenye thamani ya Tsh Milioni 954.5, miradi hii yote ipo katika sekta ya Elimu Afya, Maji,Kilimo, Mazingira na Ujenzi.

Katika Miradi hiyo Mwenge umefungua mradi wa ujenzi wa Daharia/Hosteli ya Wasichana Shule ya Sekondari Mnyigumba, umezindua mradi wa kusaidia kuhifadhi na kutunza kumazingira wa WF Renuable Resources Limited uliopo katika Kijiji cha Rungemba, Umezindua ujenzi wa Tanki la Maji mtaa wa Tanganyika, Umezindua Klabu ya Wapinga Rushwa Shule ya Sekondari JJ Mungai, Umezindua Mnara wa Kumbukumbu ya Kuuenzi Mwenge wa Uhuru mwaka 2018, Umezindua Zahanati ya Nipende katika mtaa wa Amani.   

Aidha Umeweka Jiwe la Msingi katika Ujenzi wa vyumba 02 vya Madarasa Shule ya Sekondari Ihongole, Pia umekagua mradi wa kilimo    cha zao la Parachichi mtaa wa Ndolezi na Mwisho kukagua  mradi wa Ujenzi wa Barabara ya Changarawe Matanana-Kisada yenye Urefu wa Kilometa 15 Katika mradi huu Kiongozi wa Mbio za Mwenge Kitaifa Ndugu Charles Francis Kabeho ametoa maelekezo ya kurudia kupima kwa ufanisi kama mkandarasi ametekeleza viwango vilivyowekwa katika mkataba ikiwa ni kwa lengo la kusimamia ubora wa barabara.

Akitoa Ujumbe wa Mwenge  Kiongozi wa Mbio za Mwenge Kitaifa Ndugu Charles Francis Kabeho aliwahamsisha Wananchi Kuwekeza Katika Elimu chini ya Ujumbe Mkuu wa Mbio za Mwenge 2018 “ELimu ni Ufunguo wa Maisha Wekeza Sasa kwa Maendeleo ya Taifa letu”

Pia aliendelea Kuhamasisha Kuhusu Mapambano dhidi ya Rushwa, Mapambano dhidi ya VVU/UKIMWI, Mapambano dhidi ya Madawa ya Kulevya na Mapambano dhidi ya Malaria.

Aidha alisistiza kwa viongozi wa serikali kufuatilia kwa makini miradi inayojengwa kwa ajili ya maendeleo ya wananchi ijengwe kwa ubora unaotakiwa ili thamani ya pesa inayotumika ionekane “Watumishi wote mnatakiwa kutimiza  wajibu wenu katika kulitumikia Taifa letu”alisema Kabeho    

Kwa Upande Wake Mkuu wa Wilaya ya Mufindi Mhe Jamhuri William Kupitia Risala ya Utii wa Mwenge wa Uhuru 2018 Halmashauri ya Wilaya Mufindi Kwa Mheshimiwa Rais Wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt John Pombe Magufuli Kuhusu Utekekelezwaji wa Maagizo ya Serikali katika Sekta Mbalimbali, Ikiwemo Uanzishwaji wa Viwanda, Usimamizi wa Mbolea ya Ruzuku, Kuokoa Mifumo ya Kiikoljia ya Bonde la Mto Ruaha Mkuu na Waalimu Kutojihusisha na Michango ya Wazazi Mashuleni .

Mwenge wa Uhuru Uliwashwa Rasmi na Waziri Mkuu Kasim Majaliwa Tarehe 02 Aprili 2018 Katika Mkoa wa Geita na Unatarajiwa kumaliza Mbio zake Katika Siku ya Kumbukumbu ya Baba Wa Taifa Mwalimu Julius Kambarage Nyerere na Wiki ya Vijana Kitaifa tarehe 14 Oktoba 2018 Mkoani Tanga.

                              HABARI KATIKA PICHA

Mkuu wa Wilaya Iringa Mhe Richard Kasesela aliyevaa trakisuti akimkabidhi Mwenge wa Uhuru 2018 Mkuu wa Wilaya Mufindi Mhe Jamhuri David William tayari kwa kuukimbiza katika Halmashauri ya Mji Mafinga
Kiongozi wa Mbio za Mwenge Kitaifa Ndugu Charles Francis Kabeho ajisalimiana na Mhe Mkuu wa Wilaya Mufindi Mhe Jamhuri David William
Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Mji Mafinga Bi Saada Mwaruka akisalimiana na Mmoja wa Wakimbiza Mwenge Kitaifa 2018 wakati wa Makabidhiano.


Mmoja wa wazee wa zamani waliowahi Kukimbiza Mwenge wa Uhuru miaka 50 iliyopita akiwa na Kiongozi wa Mbio za Mwenge Kitaifa Ndugu Charles Kabeho wakati wa Makabidhiano ya Mwenge baina ya Manispaa Iringa na Halmshauri ya Mji wa Mafinga katika viwanja vya Shule ya Sekondari Mnyigumba

Afisa Elimu Sekondari Halmashauri ya Mji Mafinga akisoma Taarifa ya Ujenzi wa Hostel ya Wasichana katika Shule ya Sekondari Mnyigumba
Kiongozi wa Mbio za Mwenge Kitaifa Ndugu Kabeho akikagua Ujenzi wa Hosteli na Vitanda vyake


Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Mji Mafinga Bi Saada Mwaruka akitoa maelezo ya Mradi wa Ujenzi wa Hosteli ya Wasichana Kwa kiongozi wa Mbio za Mwenge Kitaifa Ndugu Charles Francis Kabeho katika Shule ya Sekondari Mnyigumba

Kiongozi wa mbio za Mwenge Kitaifa akiweka jiwe la Uzinduzi wa Hosteli ya Wasichana Shule ya Sekondari Mnyigumba


Kiongozi wa Mbio za Mwenge ndugu Kabeho ajitoa Ujumbe wa Mbio za Mwenge 2018 mara baada ya Kuzindua Hosteli ya Shule ya Sekondari Mnyigumba







Kiongozi waMbio za Mwenge Kitaifa akikata Utepe kuashiria kuzinduliwa rasmi kwa kiwanda cha kutengeneza Mkaa kwa kutumia Mabaki ya vumbi za Mbao (Sawdust)

Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Mji Mafinga  Bi Saada Mwaruka akisalimiana na Msoma Taarifa ya Kiwanda cha Mkaa wakati Mwenge wa Uhuru ukizindua 

Kiongozi wa Mbio za Mwenge akikagua Mradi wa Kiwanda cha Mkaa na Hatua zake jinsi kinavyozalisha Mkaa huo unaolinda kuhifadhi na Kutunza Mazingira



Huu ndio Mkaa unaozalishwa na Kiwanda hiki baada ya kupitia hatu mbalimbali za Uzalishaji




Kiongozi wa Mbio za Mwenge wa Uhuru 2018 akizindua Mradi wa Ujenzi wa Tanki la Maji lenye ujazo wa lita 500,000 liliopo katika mtaa wa Tanganyika, Mjini Mafinga


Ukaguzi wa Tanki Ukifanyika





Kiongozi wa Mbio za Mwenge Kitaifa Ndugu Charles Kabeho akimtwisha ndoo ya Maji Mama aliyechota Maji kutoka kwenye bomba linaotoa maji kwenye Tanki mpya liliozinduliwa na Mwenge 2018




Baadhi ya Wananchi waliohudhuria Uzinduzi wa Tanki la Maji Uliofanywa na Kiongozi wa Mbio za Mwenge Kitaifa 2018


Kiongozi wa Mbio za Mwenge Kitaifa ndugu Charles Kabeho akizindua akiweka jiwe la msingi la Ukaguzi wa Mradi wa Kilimo cha Parachichi Unaomilikiwa na Mr& Mrs Mkisi mtaa wa Ndolezi




Kiongozi wa Mbio za Mwenge 2018 akiweka Jiwe la Msingi Mradi wa Ujenzi wa Vyumba 02 vya  Madarasa  Shule ya Sekondari Ihongole






Kiongozi wa Mbio za  Mwenge akioonge na Wananchi na Wanfunzi wa Shule ya Sekondari JJ Mungai Wakati wa Uzinduzi wa Klabu ya Wapinga Rushwa  


Akiwauliza maswali ya Ufahamu  wanafunzi wa JJ Mungai na Wanachama wa Kklabu ya Wapinga Rushwa juu  ya ulewa wa Kupinga Rushwa





Picha zote na Amani Mbwaga

Wasiliana nasi;
Mob:+255 656 632 566
Email:Prof.mbwaga@gmail.com
Twitter:@amanimbwaga

Thursday, May 24, 2018

BREAKING, ORODHA YA WANAFUNZI WA KIDATO CHA SITA WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA NA MAFUNZO YA JKT MUJIBU WA SHERIA 2018

OFFICIAL NEWS: THE LIST OF SELECTED FORM SIX LEAVER STUDENTS TO JOIN JKT 2018 NATIONAL SERVICES
 BOFYA HAPA CHINI  KWENYE ORODHA YA VIKOSI KUJUA ULIKOPANGIWA
Chanzo: JKT 

KIONGOZI WA MBIO ZA MWENGE ARIDHISHWA, MIRADI YA HALMASHAURI YA MUFINDI

Kiongozi wa Mbio za Mwenge Kitaifa Ndugu Charles Francis Kabeho Akiongea na Wananchi wa Kijiji cha  Igombavanu(Hawapo Pichani) mara baada ya Kuzindua Madarasa 02 katika Shule ya Sekondari Igombavanu

Na Amani Mbwaga Mufindi,
Jumla ya Miradi 06 yenye thamani ya shilingi bilioni 9.199 imezinduliwa, kuwekewa mawe ya msingi pamoja na kukaguliwa na Mwenge wa Uhuru, ulipokimbizwa katika Halmshauri ya Wilaya ya Mufindi, huku wakimbiza Mwenge kitaifa wakiridhishwa  na viwango vya miradi husika na kutanabaisha kuwa vinaendana na thamani ya fedha zilizotumika.

Ukiwa katika Halmashauri  ya Wilaya ya Mufindi  Mwenge wa Uhuru umeweka jiwe la msingi katika ujenzi wa vyumba vya Madarasa   Sekondari ya Igombavanu, umezindua klabu ya wapinga rushwa katika Shule ya Sekondari Igombavanu,  ujenzi wa zahanati ya Kijiji pamoja na kukagua mradi wa hifadhi ya mazingira katika msitu wa kupandwa wa Halmashauri Kijiji cha Mtili,  umezindua ujenzi wa Barabara ya lami Kitiru- Itulituli yenye urefu wa Kilometa 14.972, na mradi wa kilimo na Mifugo wa Mwananchi  kata ya Igowole.

Kiongozi wa mbio za Mwenge wa Uhuru kitaifa Ndugu. Charles Francis Kabeho, amewahamasisha wananchi kuwekeza katika elimu kwa kugharamia mahitaji muhimu ya Watoto wao, kama mavazi, viatu, Madaftari  sanjari na kuchangia michango wa Chakula cha mchana kwa wanafunzi wa kutwa  chini ya ujumbe Mkuu wa Mbio za Mwenge 2018ELimu ni Ufunguo wa Maisha Wekeza Sasa kwa Maendeleo ya Taifa letu”
Aidha, ameendelea Kuhamasisha kuhusu mapambano dhidi ya rushwa, VVU/UKIMWI, dawa za kulevya na mapambano dhidi ya Malaria.

Maambukizi ya UKIMWI yameendelea kuwa tatizo kubwa katika Mkoa wa Iringa, mkiongozwa na Mkoa wa Njombe wenye asilimia 11.4, wakati ninyi mnashika nafasi ya pili kitaifa kwa kuwa na maambukizi ya asilimia 11.3 hivyo, inatupasa tuchukue hatua za kubadili tabia kwani hali hii ikiendelea hivi ni hatari kwa maendeleo ya Taifa’’ alisema Kabeho

Kwa Upande Wake Mkuu wa Wilaya ya Mufindi Mhe. Jamhuri William, Kupitia risala ya utii  kwa mkuu wa nchi, amemuhakikishia  
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt John Pombe Magufuli kwamba, Wilaya yake, itaendelea kutekeleza  Maagizo mbalimbali ya Serikali ikiwa ni pamoja na uanzishwaji wa viwanda, usimamizi wa Mbolea ya ruzuku, kuokoa mifumo ya kiikolojia ya bonde la Mto ruaha mkuu pamoja  na suala la Waalimu Kutojihusisha na Michango ya Wazazi Mashuleni .

Mkesha wa Mwenge uliambatana na zoezi la upimaji wa maambukizi ya virusi vya UKIMWI  jumla ya watu 435 walijitokeza kujua Afya zao, kati yao wanaume ni 232 na Wanawake ni 203 ambapo katika zoezi hilo ni watu 04 tu ndio waligundulika kuwa na maambukizi ikiwa ni Wanawake 02 na Wanaume 02.

                                             HABARI KATIKA PICHA
Kiongozi wa mbio za Mwenge Kitaifa Ndugu Charles Francis Kabeho Akivishwa Skafu na Kijana wa Skauti Mufindi (Picha na Amani Mbwaga)
Mkuu wa Mkoa Iringa Mhe Amina Juma Masenza akivishwa skafu na Kijana wa Skauti Wakati wa Mapokezi ya Mwenge wa Uhuru 2018 yaliyofanyika kimkoa Katika Halmashauri ya Wilaya Mufindi (Picha na Amani Mbwaga)



Mkuu wa Wilaya Mufindi Mhe Jamhuri David William akivishwa Skafu na Vijana wa Skauti Wakati wa Mapokezi ya Mwenge wa Uhuru 2018


Kwaya Ikiimba Wakati wa Mapokezi ya Mbio za Mwenge wa Uhuru 2018




Kiongozi wa Mbio za Mwenge akisalimiana na Mkuu wa Mkoa Iringa Mara Baada ya Kumkabidhi Mwenge Ili Uweze Kukimbizwa Mkoani Iringa (Picha na Amani Mbwaga)

Kiongozi wa Mbio za Mwenge Kitaifa akisalimiana na Waheshimiwa Wabunge na Madiwani wa Halmashauri ya Wilaya Mufindi (Picha ana Amani Mbwaga)

Wakimbiza Mwenge Kitaifa mara baada ya kupokelewa Mkoani Iringa (Picha naAmani Mbwaga)


 Mkuu wa Mkoa Iringa Mhe Amina Juma Masenza akisoma Ripoti ya Mkoa kwa Kiongozi wa Mbio za Mwenge Kitaifa  aliyesimama Upande wa Kushoto kwake(Picha na Amani Mbwaga)
Kiongozi wa Mbio za Mwenge Kitaifa akisalimiana na Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya Mufindi Prof. Riziki Shemdoe (Picha ana Amani Mbwaga)



Mkuu wa Mkoan Iringa Mhe Amina Juma Masenza akimkabidhi Rasmi Mwenge wa Uhuru Mkuu wa Wilaya Mufindi Mhe Jamhuri William tayari kwa Kukimbizwa Katika Halmashauri ya Wilaya Mufindi(Picha ana Amani Mbwaga)



Wakati wa Uzinduzi wa Klabu ya Wapinga Rushwa katika Shule ya Sekondari Igombavanu


Kiongozi wa Mbio za Mwenge Wa Uhuru Ndugu Charles Francis Kabeho akipata Maelezo Kutoka Kwa Afisa Misitu wilaya ndugu Shabani Adhia Wakati akikagua Mradi wa Shamba la Miti ya Mbao la Halmashauri ya Wilaya Mufindi katika Kijiji cha Mtili

Kiongozi wa Mbio za Mwenge Kitaifa akigawa Vyandarua kwa kina mama wajawazito na wenye watoto wadogo Mara baada ya Kuzindua Zahanati ya Kijiji cha Mtili

Kiongozi wa Mbio za Mwenge Kitaifa akizindua Barabara ya Lamii yenye Urefu wa Kilometa 14.972 ya Kituli-Itulituli


Familia ya Mzee Mdemo wakipokea Mwenge wa Uhuru mara baaada ya Kukaguliwa kwa Mradi wa Kilimo na Ufugaji nyumbani Kwao Igowole (Picha na Amani Mbwaga)







 Mkuu wa Wilaya Iringa Mhe Kasesela(Kushoto) akipokea Mwenge wa Uhuru Kutoka kwa Mkuu wa Wilaya Mufindi Mhe Jamhuri David (Picha Zote na Amani Mbwaga)