Sunday, July 13, 2014

Messi na Nuer watuzwa na FIFA


Messi akipokea tuzo la ''Golden Ball''
Lionel Messi, ambaye alipoteza fursa ya kutwaa kombe la dunia aliambulia tuzo la mchezaji bora katika mchuano huo uliokamilika kwa ushindi wa Ujerumani huko Brazil.
Messi ambaye amesifiwa kwa miondoko yake na uwezo wake mbele ya lango huko Barcelona alitawazwa kuwa mchezaji bora katika mechi nne tofauti.
Messi alifunga mabao manne katika kipute hicho mbili nyuma ya mshambulizi wa Colombia James Rodriguez aliyetuzwa kuwa mfungaji mabao mengi mwaka huu.
Kipa wa ugerumani alikuwa na bahati ya kutwaa nishani ya dhahabu , kombe la dunia na pia tuzo la kipa nambari moja katika kipute hicho.
Kipa huyo mwenye umri wa miaka 28 na ambaye anayeilindia lango mabingwa wa Ujerumani Bayern Munich aliwapiku mlinda lango wa Argentina Sergio Romero na Keylor Navas kutoka Costa Rica.
Nuer akipokea tuzo la ''Golden Glove''
Neuer alifungwa jumla ya mabao 4 pekee katika mchuano huu huko Brazil.
Nuer anachukua wadhfa aliokuwa nao kipa wa Uhispania Iker Casillas.
Mshambulizi wa Colombia James Rodriguez alitawazwa mshindi wa Golden Boot baada ya kuongoza katika orodha ya wafungaji mabao mengi katika mchuano wa mwaka huu wa kombe la dunia .
Rodriguez alifunga mabao sita akifuatwa kwa karibu na Mshambulizi wa wa Ujerumani Thomas Mueller akiwa na jumla ya mabao 5.
Licha ya kuwa Colombia iliondolewa katika hatua ya robo fainali Hakuna mshambulizi aliyeweza kumpiku Rodriguez .
Nuer na Messi walituzwa
Lionel Messi, Neymar ana Robin van Persie, wote walifunga mabao manne kila mmoja.
Paul Pogba wa Ufaransa alituzwa kuwa mchezaji anayeinukia bora .
Timu ya Colombia ilituzwa kwa kuwa timu yenye nidhamu katika mashindano haya

Source: BBC.

UJERUMANI YAIBUKA BINGWA WA KOMBE LA DUNIA 2014 DHIDI YA ARGENTINA.



Hatimaye fainali za kombe la dunia zilizo anza rasmi tarehe 12/06/2014 kule nchini Brazil zimefikia tamati usiku huu, huku timu ya Ujerumani ikiibuka mshindi wa kombe la dunia 2014 baada ya kuifunga timu ya  Argentina goli 1-0 katika dakika za nyongeza, mnamo dakika ya 110.

Mtanange huu wa fainali uliokuwa mkali huku timu zote zikishambuliana kwa zamu, hatimaye timu ya Taifa ya Ujerumani imeweza kuibuka kidedea baada ya mchezaji Mario Gotze wa Ujerumani kuifungia timu yake ya Taifa goli pekee na kuiwezesha Ujerumani kuwa mabingwa wapya wa kombe hili dhidi ya wapinzani wao Argentina, mechi hii imechezwa katika dimba la  Maracana jijini Rio de Janeiro.

                                             Kikosi cha timu ya Taifa ya Ujerumani
Wunderbar: Germany's Mario Gotze scored with a brilliant finish to put his team ahead in the dying minutes of the World Cup final against Argentina tonight
 Mario Gotzeakitupia goli pekee la ushindi.
 
Goal! Mario Gotze of Germany scores his team's first goal past Sergio Romero of Argentina in extra time
Goal! Mario Gotze akiipatia Ujerumani goli la ushindi.

Vital goal: Gotze celebrates with (left to right) Andre Schuerrle, Benedikt Hoewedes and Thomas Mueller after scoring during extra-time
Muller, Gotze wakishangilia goli.

The agony and the ecstasy: While the Germans celebrate Gotze's goal, the Argentine players seemed stunned to have conceded so late on
On a wing and a flare: German fans celebrate as the final whistle blows in the Maracana stadium

Elated: After nervously seeing out the final moments of the game, the German team and their fans burst into wild celebrations as the final whistle blew

Champions: German fans wave replica trophies in the air as they celebrate their team's famous win

Mashabiki wa Ujerumani.

Source: Nyanja

LUIZ FELIPE SCOLARI ANA `ROHO YA PAKA`, HII NDIO KAULI YAKE BAADA YA KUCHAPWA 3-0 NA UHOLANZI!!


434667_heroa
LUIZ Felipe Scolari amesema hatajiuzulu katika nafasi yake ya ukocha wa timu ya taifa ya Brazil, licha ya timu yake kufungwa mara ya pili mfululizo ndani ya siku tano.
Brazil walifungwa mabao 7-1 katika mechi ya nusu fainali iliyopigwa Belo Horizonte siku ya jumanne ya wiki hii na usiku wa jana walifungwa mabao 3-0 na Uholanzi na kumaliza katika nafasi ya nne ya fainali za 2014 za kombe la dunia kwenye ardhi yake.
Kabla ya mashindano haya, Brazil  ilikuwa haijapoteza mechi nyingi za nyumbanii tangu mwaka 2002 na walikuwa hawajawahi kufungwa nyumbani katika mashindo ya mpira wa miguu tangu mwaka 1975, lakini kufungwa mara mbili mfululizo ndani ya siku tano kumewachangaya mashabiki  na waandishi wa habari wan chi hiyo.
Lakini Scorali alikutana na waandishi wa habari baada ya kufungwa na Uholanzi na kusisitiza kuwa shirikisho la soka nchini Mbrazil litaamua hatima yake ya baadaye.
“Ulikuwa mchezo wenye nguvu sawa,” alisema. “Wachezaji wanatakiwa kupongezwa kwa jinsi walivyocheza. Hatukucheza vibaya-hayo ndio maoni yangu”.
“Kwasasa sio muda muafaka wa kuzungumzia hilo, “ alisema Scolari. “Nitaandika ripoti yangu na kumwambia rais wa CBF ni kitu gani nadhani hakikwenda sawa, yeye ataamua nini anataka kwa baadaye. Tumepoteza mechi nyingine, lakini maisha yanaendele”.
“Mwaka mmoja uliopita nilishinda kombe la mabara,” aliongeza. “Makosa hayako kwa makocha. Kitu ni kwamba tuna timu ya vijana sana. Hatujazalisha wachezaji wa kutosha, kwahiyo sio kazi rahisi hata kama Kocha mwinine atakuja”.
Source: shafii Dauda. From Brazuka.

Friday, July 11, 2014


Mwandishi wa makala hii ni mhadhiri msaidizi na mkuu wa Idara ya mawasiliano na uandishi wa habari Chuo Kikuu Kishiriki cha Mt. Agustino cha Tanzania (SAUT) Songea. Anapatikana kwa denis_mpagaze@yahoo.com, 0753665484 au unaweza kusoma makala zake kupitia ukurasa wake wa facebook Denis Mpagaze 

Ubabe, dharau, kejeli na unafiki ni dhambi ambazo zinalitafuna Taifa letu kwa kasi zaidi ya upepo. Nchi yetu imegeuka kuwa kisima cha ubabe, vitisho na dharau. Kitendo cha Mbunge wa Kasulu kuhoji mstakabali wa nchi yetu na kuitwa tumbili ni ubabe, dharau na kejeli. Kitendo cha wananchi wa Kigamboni kuhoji uhalali wa kuongezeka kwa nauli ya kivuko na kuambiwa asiyeweza kulipa apige mbizi ni dharau. Kitendo cha wananchi kuambiwa maji sio mkojo kupatikana kila sehemu ni kebehi. Kitendo cha wananchi kuuliza uhalali wa kigogo kutumia ndege ya serikali na kujibiwa mlitaka atumie punda ni majivuno. Kitendo cha waandishi wa habari kuhoji mstakabali wa nchi yetu na kuishia kung’olewa kucha na meno bila ganzi ni vitisho. Kitendo cha kusimama Bungeni na kukosoa bajeti na baadaye kuunga hoja kwa asilimia zote ni unafiki. Kitendo cha kuwaambia watanzania asiyeweza kulipia umeme atumie kibatari ni dharau. Mwisho wa dhambi hii siku zote hushangaza. Kwa nini nasema hivi? 

Robert Kiyosaki kupitia kitabu chake cha Rich Dad Poor Dad anasema kwamba historia ni mwalimu mzuri. Ni historia inayonipa nguvu na ujasiri kusema kwamba matokeo ya ubabe, dharau, unafiki na kejeli siku zote hushangaza. Bas twende pamoja katika kuthibitisha kauli yangu kwa kurejea kumbukumbu katika historia. 

Katika kitabu chake kiitwacho, “A Night to Remember”cha mwaka 1976, uk 73 Walter Lord ameonesha dharau na majivuno aliyokuwanayo mbunifu wa meli ya Titatic. Mbunifu huyo alipoulizwa na waandishi wa habari kuhusu usalama wa meli hiyo kubwa kuwahi kutokea, alijibu “meli hiyo ni kubwa kiasi ambacho hata Mungu hawezi kuizamisha”. Matokeo ya kauli hii yaliishangaza dunia. Meli hiyo ilizama na kuacha huzuni kuu. Na hili ni funzo kwa viongozi mliojaa dharau na mizaa mpaka kumkufuru hata Mungu. Acheni!

Mobutu Sese Seko Kuku Ngbendu wa Za Banga baada ya kuwa rais wa kwanza Afrika kupata misaada mingi kutoka USA aliota kiburi na majivuno. Aliitangazia Dunia kwamba yeye ni kuku anayeatamia nchi ya Congo wakati huo ikiitwa Zaire. Huwezi amini kwa dharau zake alijifananisha na Mungu. Kabla ya taarifa ya habari, luninga ya Taifa ilionesha picha yake akishuka kutoka mawinguni na watu wote walikaa kimya kumlaki mtukufu Mobutu Sese Seko Kuku Ngbendu wa Za Banga. Ni kufuru. Alijenga majumba ya kifahari kila kona ya Dunia wakati mamilioni ya wakongo wakiishi maisha ya Kanyaga Twende. Ni ushenzi. Mwisho wake ulishangaza sana. Alifariki akiwa uhamishoni Rabat, Morocco kwa ugonjwa wa kansa akiwa na umri wa miaka 66, na kuzikwa na watu wanne tu. Hili ni funzo kwa viongozi wenye tabia za Mobutu Seseko. Acheni!

Yuko wapi Saddam Hussein, mbabe aliyoitikisha Dunia mpaka kututia hekaheka ya kuchimba mahandaki kila kona ya nchi yetu. Wengi mnakumbuka. Alitishia kulipua visima vya mafuta ambavyo madhara yake yangekuwa kuiangamiza Dunia. Huu ulikuwa ubabe. Je mnaukumbuka mwisho wake? Pamoja na ubabe wake, alikuja kukamatiwa kwenye shimo mithili ya panya aliyemkimbia paka. Inashangaza na pengine inaweza kuwa funzo kwa viongozi wababe ndani ya nchi yetu kama Saddam. Mbabe siku zote hana rafiki. 

Yuko wapi Adolf Hitler aliyemfananisha mtu mweusi na nyani pale alipowashinda wazungu katika mbio za Olympic. Hitler alikataa kumpa mkono jamaa yetu kwa husema haiwezekani binadamu kushindanishwa na nyani. Hii ilikuwa ni kufuru na chukizo kwa Mungu. Nampenda sana hayati Luck Dube, kwa maneno yake matamu, “When I see a black man...I see the image of God, when I see a white man...I see the image of God, I see an Indian...I see the image of God, colours and everybody, we are the images God”, Ni hekima za Lucky Dube .Mwisho wa Hitler nadhani kila mtu anaufahamu. Unashangaza! Hata kaburi lake halijulikani liko wapi. Hili nalo ni funzo kwa viongozi wa namna hii.

Yuko wapi Jonas Savimbi, dikteta wa Angola aliyewakata vidole watoto wetu ili wasije kumpindua madarakani ? Leo vijana wengi huko angola hawana vidole. Ni ubabe huu. Ukiambiwa kifo chake utashangaa. Alifia barabarani na maiti yake kuburuzwa mji mzima kama mzoga wa mbwa kabla ya kuzikwa chini ya mti. Inashangaza. Chukua funzo hili kama ni miongoni mwa viongozi wababe na wenye roho mbaya. Kitendo cha kuuza madawa ya kulevya ni kuwakata vidole watanzania. Acheni!
Yuko wapi aliyewatandika walimu wa shule ya msingi viboko huko Bukoba? Kwa mara ya mwisho nilimsikia kachoka mbaya.Siyo mkuu wa wilaya tena. Ni madhara ya kutumika. Leo hii kiongozi unasimama juu ya majukwaa na kuanza kuporomosha matusi, kejeli na maudhi, kisa umekubali kutumika. Nakwambia we endelea tu, matokeo yake yatakushangaza. Nadhani hili ni funzo kwa wale wote wanaotumika kwa maslahi ya wachache! Acheni!

Yuko wapi Benito Monsoln, aliyekuwa akiwaweka roho juu wachezaji wa Mpira huko Italia kila ilipokaribia kombe la Dunia? Aliwaambia kama hawatachukua Kombe la Dunia atawachinja wote. Ni vitisho hivyo. Leo pamoja na vitisho vyake anarutubisha ardhi ya Italia. Narudia tena, mwisho wa ubabe na vitisho unashangaza. 

Yuko wapi Idd Amin aliyewalazimisha watu kucheka na walioshindwa kucheka aliwakata midomo na meno kubaki nje mithili ya mtu anayecheka? Leo hayupo tena. Kafa kifo cha aibu uhamishoni . Inashangaza. Bado tu hamjifunzi?
Nawakumbusha viongozi wenye kauli za kibabe, maudhi na kinafiki kwamba matokeo yake yatawashangaza. Wakumbuke kwamba kwa ubabe wao,watanzania tunadhoofika, kwa unafiki wao watanzania tunasalitiwa, kwa majivuno yao watanzania tunaumia, kwa dharau zao watanzania tunaugua. Hata maneno ya Mungu yanasema kupitia Mithali 29:2,b; "bali mwovu atawalapo,watu huugua". Mwaka 2011 jijini Dar Es Salaam aliyekuwa rais wa awamu ya tatu alisema, “kuwa na viongozi wasiokuwa waadilifu kunasababisha kuwa na Serikali za hovyo zisizojali matakwa ya wananchi”. Kutojali wananchi ni ubabe, dharau, kejeli na unafiki. 

Najua kinachowasumbua ni ulevi na ulimbukeni wa madaraka kama alivyowahi kusema mtaalam wa uandishi wa riwaya, George Orwell, kuwa, “Power corrupts and absolute power corrupts absolutely”akimaanisha madaraka yakizidi hulevya. Hakika viongozi wetu wamelewa kwa ukubwa wamadaraka na wananchi wamelewa kwa mizigo ya umaskini na kero. Inashangaza! 

Bila kujalisha nani kalewa nini na kwa sababu gani, ukweli ni kwamba, Dunia haitakukumbuka kwa ubabe wako, kwa unafiki wako, kwa kejeli zako, kwa dharau zako, kwa majivuno yako, bali itakukumbuka kwa namna matendo yako mema yamevyogusa nyoyo za watu. Leo mpaka wapinzani bila kujali itikadi zao wanamkumbuka Mwl Julius Nyerere, wanamkumbuka Mahatma Ghandi, wanamkumbuka Nelson Mandela. 

Watu hawa wanakumbukwa kwa sababu ya matendo yao mema na si kauli za kibabe, kinafiki na kujipendekeza. Ni watu ambao walikuwa tayari kufa kwa ajili ya watu. Alipopigwa teke la mdomoni na askari wa kikaburu kule Afrika kusini, Mahtma Ghandi aliinuka na kujifuta mavumbi na kuuliza, “Afande, hivi kiatu chako kimepona? Pamoja na kuwekwa jela miaka 27 bado Nelson Mandela aliwasamehe adui zake na kuwa tayari kufanya nao kazi. Baada ya kuusotea uhuru wa Tanganyika kwa muda mrefu bado Nyerere alijiona hayuko huru mpaka Afrika yote iwe huru. Alianza harakati. Wote mnakumbuka. Mpende jirani yako kama nafsi yako, hakika utakumbukwa daima. 

Kijana mmoja alikuwa akisafiri kwa basi. Wakati wa safari alikuwa anafoka na kutukukana watu hovyo. Wakati anashuka, abiria mmoja akamwambia, “Kijana umeacha kitu”. Kijana akauliza kwa ukali. “Nimeacha nini?” Abiria akamwambia umeacha jina chafu.

Nachotaka kusema ni kwamba, tunaelekea uchaguzi wa serikali za mitaa na uchaguzi mkuu hivi karibuni, nakuomba msomaji wangu bila kumung’unya maneno, muulize mbunge wako, diwani wako, mwenyekiti wako wa mtaa na rais wako ameacha jina gani kabla hajaomba ridhaa tena ya kukutawala. Nyie ulizeni maswali hayo tu na mtaona matokeo yatakavyoshangaza!

Source: Nyanja poti Blog.

Thursday, July 10, 2014

HESLB: Hii ndio mbinu mpya kuwabana wanaokwepa kurejesha mikopo ya wanafunzi wa elimu ya juu.



Serikali imetangaza kuwa haitawaruhusu wahitimu wa elimu ya juu wanaodaiwa na Bodi ya Mikopo ya Elimu ya Juu (HESLB) kwenda nje ya nchi kwa masomo zaidi au kufanya kazi mpaka watakapomaliza kulipa madeni yao.

Akizungumza bungeni hivi karibuni, Naibu Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi, Jenista Mhagama alisema hatua hiyo inalenga kuongeza kiwango cha ukusanyaji wa mikopo ambayo imeshawanufaisha wahitimu wengi ingawa ni wachache wanaorejesha.

"Tumezungumza na idara ya uhamiaji ili wale wote wanaotaka kwenda kufanya kazi nje ya nchi wasiruhusiwe mpaka watakapomaliza kulipa mikopo yao ya elimu ya juu. Lengo ni kuepuka ukwepaji unaojitokeza baada ya kuajiriwa," alisema.(Martha Magessa)
Suala la wahitimu wa Kitanzania kutafuta kazi nje ya nchi limekuwa likizungumzwa na wadau wengi kama njia mbadala ya kupata ajira, kutokana na kuwapo kwa ushindani mkubwa wa soko la ndani la ajira.

Wahitimu
Hata hivyo, baadhi ya wadau hawaoni manufaa endelevu ya mpango huo, wakisema chombo kinachohusika na mikopo hakijajipanga vilivyo kukusanya madeni na ndiyo maana kimeshindwa kuwafikia hata wadaiwa waliomo nchini.

Leonard Mhongole ni mhitimu wa Chuo Kikuu cha Ardhi mwaka 2010. Anasema mkakati huo hauwezi kuleta tija kwa kuwa ni watu wachache sana wanaofikiria kwenda nje ya nchi.
"Mamlaka husika zinaangalia sana waajiriwa wa serikalini lakini kwa wale tunaofanya kazi sekta binafsi au waliojiajiri hatufikiwi. Kama watu wote watabanwa kama inavyotakiwa nadhani fedha za kutosha zitarudi serikalini," anasema na kuongeza:
"Mimi binafsi nilitakiwa niwe nimeanza kulipa mkopo wangu lakini kwa kuwa hakuna anayenitaka kufanya hivyo siwezi kuwatafuta wahusika...inawezekana wametoa msamaha kwa baadhi ya watu."

Kwa upande wake, mwanafunzi wa shahada ya uzamili katika Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, Joseph Isindikiro, anasema utekelezaji wa mkakati huo ni ukiukwaji wa haki ya msingi ya mtu kupata elimu.
"Mpango huo hautawezekana kwa sababu serikali yenyewe imekiri kuwa kuna tatizo la ajira na kupendekeza wahitimu kuomba kazi nje ya nchi. Sasa itakuwaje wao wenyewe wazuie ilhali wanajua mhusika hana uwezo huo na ajira hiyo ndiyo tegemeo lake?" anahoji.

Anaongeza kusema kuwa kufanya hivyo ni sawa na kumtia mtu hatiani kutokana na haki yake ya kupata elimu kama inavyobainishwa katika Katiba.
CHANZO:MWANANCHI

Sunday, July 6, 2014

WATU ZAIDI YA 50 WAUAWA UGANDA


Watu wasiopungua 50 wameuawa baada ya watu wenye silaha kushambulia vituo vya polisi na kambi za jeshi nchini Uganda, kwa mujibu wa jeshi.
Miongoni mwa waliokufa ni washambuliaji 41 na polisi pamoja na raia 17.
Mashambulio hayo yametokea magharibi mwa Uganda, karibu na mpaka na Jamhuri ya Kidemokrasi ya Kongo.
Mashambulio hayo yamelenga majeshi katika wilaya za Kasese, Ntoroko na Bundibugyo.
Msemaji wa jeshi amesema mashambulio hayo hayana uhusiano wowote na kundi la waasi la ADF, ambalo lilikuwa likifanya shughuli zake katika eneo hilo zaidi ya muongo mmoja uliopita.
"Tunachofahamu ni kuwa wanamgambo hawa hawana uhusiano na ADF-NALU, lakini tunachunguza kuona sababu hasa na nani wanawaunga mkono," amesema Paddy Ankunda, msemaji wa jeshi akizungumza na shirika la habari la Reuters.
Watu 17 walikamatwa na wanahojiwa kwa mujibu wa polisi.
LikeSource: kikeke S.