Saturday, July 1, 2017

JKT Kuongeza Idadi ya Vijana Vikosini.

Mahafali ya Ufungaji wa Mafunzo ya Awali ya Kijeshi Oparesheni Magufuli Kujitolea Mafinga JKT, Tarehe 28 Juni, 2017.                                                                                                                                       
Vijana wa Mafinga JKT Wakitoka nje ya Uwanja mara baada ya kumaliza Gwaride la Kuhitimu Mafunzo yao ya awali ya Kijeshi Tarehe 28 Juni 2017


Mgeni Rasmi Mkuu wa wilaya ya Mufindi Jamhuri David William Akipokea Salamu ya Heshima Kutoka kwa Gwaride lililoandaliwa na Vijana wa Mafinga JKT Oparesheni Magufuli Kujitolea wakati wa Kuhitimu Mafunzo yao ya awali ya Kijeshi.
Na Amani Mbwaga                                                   
Mafinga, Tanzania.
Jeshi la kujenga Taifa JKT limejipanga kidete kuongeza idadi ya vijana wa Tanzania kujiunga na Mafunzo ya awali ya kijeshi, baada ya kufufua Vikosi na Makambi ya awali ya Jeshi hilo.

Hayo yamesemwa na Mwakilishi wa Mkuu wa JKT Luteni Kanali AS Kagombola ambaye  ni Mkurugenzi wa Ustawi wa Jamii JKT, alipokuwa akitoa salamu kwa niaba ya Mkuu wa Jeshi hilo Meja Jenerali Michael Isamuhyo, wakati wa kufunga mafunzo ya awali ya kijeshi ya Kundi Magufuli katika Kikosi cha Mafinga JKT, Kilichopo wilaya ya Mufindi Mkoani Iringa.

Mkuu wa JKT amempongeza Mh Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt John Pombe Magufuli kwa kuona umuhimu wa vijana na  kufufua vikosi hivyo vya JKT.

Tarehe 15 Machi 1967 Kikosi cha Mafinga JKT Kilifunguliwa rasmi kikiwa na vijana wachache ambao walijiunga kufanya shughuli za kujenga Taifa.
Baadhi ya sababu za kuanzishwa kwa JKT ni Kubadili fikra za Vijana wa nchi hii kutoka ile hali ya ukoloni ya kutegemea nchi nyingine ili kuleta Maendeleo, Kuwafunza Vijana Kujenga Mshikamano na umoja wa kitaifa ili kulinda uhuru wa Taifa lao.

Pia ni kuwaunganisha vijana bila kujali itikadi zao, kujifunza uzalendo na stadi za maisha ili waweze kujiajiri na kujitegemea mara wamalizapo mkataba wao wa kujitolea kwa miaka miwili.

Luteni Kanali Kagombola alisema, “katika kutambua hilo Serikali imerejesha Makambi Matano (05) yaliyokuwa yamesitishwa kufanya mafunzo,  ili kuongeza zaidi uwezo wa Kuchukua Idadi kubwa ya Vijana” Makambi yaliyofunguliwa ni 826 KJ Mpwapwa Dodoma, 839 KJ Makuyuni Arusha, 845 KJ Itaka Songwe, 846 KJ Luwa Rukwa, 847 Milundikwa Rukwa, wakati huohuo Makuyuni Arusha tayari imeshaanza kuchukua vijana na sasa wanaendelea na mafunzo.

Kwa upande wake Mkuu wa Wilaya ya Mufindi Mhe Jamhuri David William ambaye alikuwa Mgeni Rasmi na Kufunga Mafunzo hayo amewataka vijana kufanya kazi kwa bidii, Uhodari,Uadilifu  na Weledi wa hali ya juu mara wapatapo nafasi za ajira katika vyombo vya ulinzi na usalama.

“Aidha kwa wale watakaomaliza mkataba wao wa JKT na kurudi nyumbani nawataka mkawe raia wema na kamwe msijiingize katika mambo ya uhalifu na ujambazi, bali mkashirikiane na jamii kwa yale mazuri mliyojifunza hapa Jeshini ili kuilinda nchi yetu na kuleta maendeleo kwa Taifa letu” alisema Mhe Jamhuri William.

Naye Mkuu wa Kikosi cha Mafinga JKT  Luteni Kanali Hamis Maiga aliwashukuru wahitimu wa kundi la Magufuli Kujitolea kwa kuwa na nidhamu kubwa wakati wote wa Mafunzo yao ya miezi sita.

Alisema Kikosi Kimepata vijana waadilifu wenye nidhamu na Ubunifu wa hali ya juu, kwani wametuachia Mashine ya Kusaga Nafaka na kupaki unga, Bwawa kubwa la Ufugaji wa Samaki  na mengine mengi.

Wito wake kwa vijana hawa wa JKT ni kutunza kiapo walichoapa cha Uhodari, Utii na Uaminifu, kwa lengo la kubadilisha changamoto zilizopo katika jamii na kuzibadili kuwa fursa.

Serikali ilirejesha Mafunzo ya JKT Kwa vijana wa Kujitolea mwaka 2001 baada ya kusitiswa mwaka 1994.
Oparesheni katika Mafunzo ya JKT zilizowahi kupita Toka 2001 ni:

Oparesheni Mkapa             2001
Ø Miaka 40 ya JKT                 2002
Ø Utandawazi                          2004
Ø Jiajiri                                    2005
Ø Kasi Mpya                             2006
Ø Maisha Bora                          2007
Ø Uadilifu                                  2008
Ø Kilimo Kwanza                      2009
Ø Uzalendo                                2010
Ø Miaka 50 ya Uhuru                2011
Ø Sensa                                      2012
Ø Miaka 50 ya JKT                    2013
Ø Miaka 50 ya Muungano          2014
Ø OP Kikwete                             2015
Ø OP Magufuli                            2016- Hadi Sasa.



                                      HABARI KATIKA PICHA.

Mgeni Rasmi Mkuu wa Wilaya ya Mufindi Jamhuri David William akitoa hotuba  kwa Hadhira iliyohudhuria Mahafali ya Kuhitimu Mafunzo ya Awali Ya Kijeshi Katika Kikosi cha Jeshi  Mafinga
Mwakilishi wa  Mkuu a JKT Luteni Kanali AS Kagombola ambaye pia ni Mkurugenzi wa Ustawi wa Jamii JKT akijiandaa kutoa Salamu za Mkuu wa JKT

Kamanda  Kikosi wa Kikosi cha Jeshi Mafinga Luteni Kanali Hamis Maiga akitoa wito kwa vijana waliomaliza mafunzo ya awali ya Kijeshi, Kundi la OP Magufuli Kujitolea.
Kamanda Kikosi Luteni Kanali Hamis Maiga akimtambulisha Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Mufindi Prof:Riziki Shemdowe
Paredi Kamanda Kapteni  Bakari Namgugu Akimshukuru Mgeni Rasmi Mara baada ya Kumaliza Ukaguzi wa Gadi za Maonesho ya kwata ya Mwendo wa Pole Na Haraka, katika Mahafali ya Vijana  JKT Oparesheni Magufuli Kijitolea Katika Kikosi cha Jeshi Mafinga.











BrassBand ya Mafinga JKT Ikitulia wakati wa Ukaguzi wa Mgeni Rasmi Mkuu wa wilaya ya Mufindi wakati wa Mahafali ya Kumaliza Mafunzo ya awali ya Kijeshi Kikosini Hapo.

Gwaride likitoka nje ya Uwanja.


Baadhi ya Ndugu , Jamaa, Marafiki na Wananchi wa Mkoa wa Iringa Wakifuatilia Kwa Makini Sherehe  Za Kumaliza Mafunzo ya Awali ya Kijeshi Katika Kikosi Jeshi Mafinga.

Kikundi cha Singe


Kikundi cha Sarakasi cha Mafinga JKT








Mgeni Rasmi Mkuu wa Wilaya ya Mufindi Katikati akiwa katika Picha Ya Pamoja na Wakuu   mbalimbali wa vikosi vya Jeshi waliosimama nyuma.
Mgeni Rasmi akiwa katika picha ya Pamoja na Kamati Tendaji ya Kikosi cha Jeshi Mafinga




Mgeni Ramsi akiwa Katika Picha Ya Pamoja Viongozi wa Serikali ya Vijana Op Magufuli


Bwawa la Ufugaji wa Samaki la Kikosi cha Jeshi Mafinga Unaosimamiwa na Vijana wa Kujitolea  Mafinga JKT

Vijana wa JKT Mafinga (SM) Oparesheni Magufuli wakilisha Samaki Chakula

Kijana wa JKT (SM) Oparesheni Magufuli akiwapa elimu ya Ufugaji wa Samaki Wazalendo wa Mujibu waSheria waliomaliza Kidato cha Sita Mwaka Huu.


Jengo la Kiwanda Kidogo cha Kusaga nafaka na Kupaki Unga Bora Cha Mafinga JKT.

Kwa Mawasiliano Zaidi.
Mob: + 255 656 632 566
           :+  255 765 058 711
Twiter:@amanmbwaga






No comments:

Post a Comment