Wednesday, November 28, 2018

Wizara ya Maliasili na Utalii Yanuia Kusomesha Wataalamu wa Ukuzaji wa Mbegu za Miti nchini


Na Amani Mbwaga.

Hayo yamesemwa na Katibu Mkuu wa Wizara ya Maliasili na Utalii Profesa Adolf Mkenda alipofanya ziara yake ya kwanza Wilayani Mufindi Mkoani Iringa  kuja kufanya kikao na Bodi ya programu ya Panda Miti Kibiashara (Private Forest Programme) inayofadhiliwa na Serikali ya Finland ambapo Mwenyekiti wake ni Katibu Mkuu wa wizara na Balozi wa Finland.

“Tumekubaliana kwamba tutahakikisha tunatenga fedha za kusomesha watanzania wenye taaluma hii ya ukuzaji miti (Tree Breeding) twende Sokoine pale watu wenye digrii ya kwanza ya misitu tuwafadhili waende wakasome digrii ya Uzamili (Masters) kwenye maeneo haya ikiwezekana tuwapeleke kwenye nchi ambazo zimebobea kama vile Finland illi wakirudi hapa waje hapa kutusaidia” alisema Prof. Mkenda

Prof Mkenda amebainisha kwamba pamoja na jitihada za kuwa na wakala wa mbegu za miti Tanzania(TTSA) bado kuna tabia ya kununua mbegu nyingi sana kutoka nje ya nchi na sababu ya kufanya hivyo ni kwamba ili upate mbegu bora ni lazima uwe na kitalu cha kuzalisha mbegu ili kuotesha miti ya majaribio na uwe na wataalamu.

“Naamini tunafursa kubwa ya kuwa wazalishaji wakubwa wa mbegu na kuziuza ndani na nje ya nchi lakini tuanataka kuamini kwamba program kama hii ya Panda miti kibiashara itakapoondoka tubaki na uwezo fulani wa kujiendeleza sisi wenyewe kwanza kwenye vijiji vyetu”,alisema Prof Mkenda

Aidha amesema walichokiona Mufindi kupitia shamba linalomilikiwa na kijiji la uzalishaji wa mbegu za miti  na mashamba  mengine kumilikiwa na wanakijiji wenyewe wamejifunza kitu kikubwa sana na kitaingia katika sera ya misitu ambayo inakamilishwa hivi karibuni wa ajili ya kuizindua mwakani.

Kabla ya kampeni ya Kitaifa ya kupanda miti vijijini                            (Village Afforestation Programme) kuanza rasmi mwaka 1970 kwa kiasi kikubwa jukumu la kupanda miti na kusimamia misitu lilikuwa la serikali kupitia idara ya misitu na nyuki mfano wa shamba la Miti Sao Hill, wakati wa kampeni hiyo wananchi na taasisi mbalimbali zilihusishwa na kuhimizwa kushiriki katika upandaji miti kwa ajili ya matumizi mbalimbali chini ya dhana ya misitu ya jamii (Community Forestry)

Kwa Upande wake Mkuu wa Wilaya Mufindi Mhe Jamhuri William ameishukuru sana serikali ya awamu ya tano inayoongozwa na Rais makini kwa kutoa muongozo mzuri mzuri sana kwa kushirikianana Panda miti kibiashara (PFP) Katika kutekeleza miradi mbalimbali ya kupanda miti.

“Tumeona katika maeneo mengi wameshirikiana na serikali katika mipango ya matumizi bora ya ardhi” alisema Mhe William.

Aidha Mshauri wa sekta binafsi ya misitu Tanzania Bwana Sangito Sumari amesema katika shamba la mbegu lililopo katika kijiji cha Holo ambalo lilianzishwa na program ya panda miti kibiashara chini ya ufadhili wa Serikali ya Finland kupitia wizara ya maliasili na utalii.

Shamba hilo limepandwa toka Januari 2015 na tayari limeshaanza kutoa matunda ambayo yataweza kuzalisha mbegu ambazo ni bora zitakazosaidia wakulima wa miti.

Madhumuni hasa ya Panda miti kibiashara ni kushughulika haswa na mnyororo mzima wa sekta ya misitu kuanzia mbegu bora, utunzaji wa misitu, uuzaji, uchakataji na utafutaji wa masoko ili kuwawezesha wakulima wa mazao ya miti ili wapate mbegu bora.

Mradi wa panda miti kibiashara (PFP) ulianza rasmi mwaka 2014 na kufikia Zaidi ya vijiji 59 lakini pia kupanda miti zaidi ya hekta 12000 na hizi zinajumuisha wakulima wadogo wadogo ambao wanafikia karibu ya wakulima 6000 ambao wanamiliki mashamba yao binafsi kupitia vikundi vyao alisema Bwana Sangito.

Takwimu zinaonesha kuwa eneo la misitu ya asili hapa Tanzania ni hekta 48,000,000 na misitu ya kupandwa ni hekta 553,000.

Kutokana na sera ya Taifa ya misitu ya mwaka 1998 sera ya Taifa ya hifadhi za mazingira ya mwaka 2004 na program mbalimbali za kuhamasisha upandaji miti kila mwaka, ni dhahiri kuwa serikali inahimiza wananchi na taasisi zishiriki kikamilifu katika suala la kupanda miti.

HABARI PICHA

Prof. Adolf Mkenda akiongea na Wanufaika wa Mradi wa Panda Miti Kibiashara katika Kijiji cha Lugolofu Wilayani Mufindi 
Balozi wa Finland Nchini Bwana Pekka Hukka

Kushoto Katibu Mkuu Wizra ya Maliasili na Utalii akisalimiana na Mkuu wa Wilaya Mufindi Mhe Jamhuri William


Dkt. Ezekiel Mwakalukwa Mkurugenzi wa Misitu na Nyuki Wizara ya Maliasili na Utalii

Mshauri wa sekta binafsi ya misitu Tanzania Bwana Sangito Sumari


Kuelekea Mgololo Escarpment

Prof Mkenda akioneshwa ramani ya miradi inayotekeelezwa na Panda Miti Kibiashara








Mmoja wa wamiliki wa shamba la miti na Mnufaika wa mradi wa Panda Miti Kibiashara



Mtalamu wa Uandaaji wa mbegu katika Mradi waPanda mitiKibiashara Bwana Christopher Komakech akitoa maelezo ya kitalu cha shamba la kuotesha mbegu

Shamba la Kuandaa Mbegu za Miti Katika Kijiji cha Holo Wilayani Mufindi linalofadhiliwanamradi wa panda miti kibiashar huku likimilikiwa na Wanakijiji wa kijiji hicho



Prof Mkenda Kulia na Kushoto ni Mshauri wa Sekta binafsi ya misitu Tanzania Bwana Sumari wakiteta jambo. 




Prof. AdolfMkenda akisalimiana na Mwezeshaji wa Panda iti kibiashara wa kijiji cha Lugolofu Bwana Adolf  Ngilangwa




Bwana Ngilangwa Akisoma Taarifa ya Mradi





Mwenyekiti wa Kijiji cha Lugolofu akimweleza jambo Bwana Sumari




Prof. Mkenda akisalimana na Mwenyekiti wa Kijiji cha Lugolofu






Picha ya Pamoja (Picha zote na Amani Mbwaga)

Monday, November 26, 2018

NAIBU WAZIRI WA NISHATI SUBIRA MGALU AFANYA ZIARA YA KUTEMBELEA CHANZO CHA UMEME MWENGA MIN HYDRO POWER NA KUWASHA UMEME IKONGOSI-MUFINDI.


Na Amani Mbwaga.
Naibu Waziri wa Nishati, Subira Mgalu amewasha umeme katika kijiji cha Ikongosi na Kufanya ziara ya kutembelea chanzo cha Umeme kutoka kwa Mzalishaji binafsi MWENGA HDRO POWER Chini ya Kampuni tanzu ya RIFT VALLEY ENERGY iliyopo wilayani Mufindi Mkoani Iringa.

“Nimefurahi kufika Mwenga hapa na nadhani ni mradi wangu wa kwanza kufika katika mradi kama huu wa sekta binafsi  tangu nimeteuliwa kuwa naibu waziri wa Nishati katika uzalishaji huu wa umeme kwa kutumia maporomoko ya maji, nawapongeza sana Mwenga”. anasema Mhe Mgalu

Katika suala la uhifadhi mazingira Mhe Mgalu ameitaka kamati ya ulinzi na usalama ya wilaya ya Mufindi kuchukua hatua za makusudi ili kuhakikisha vyanzo vya maji ikiwemo chanzo cha mto mwenga vinatunzwa ipasavyo ili kuwa na umeme wa uhakika na wale wanaofanya shughuli za kilimo karibu na vyanzo vya maji waondolewe mara moja bila kuoneana haya.

“Tupo katika vita ya kuhakikisha miradi inayozalishwa kwa kutumia umeme inafanya kazi kama ilivyokusudiwa, nashukuru mungu mwaka huu hatujaona athari katika Mtera na Kidatu” alisema Mhe Mgalu.

Akitoa wito kwa wakazi wa maeneo ya chanzo cha umeme wa maji Mwenga, amewataka wananchi  kuendelea kutii maagizo ya serikali za mitaa ya kutunza vyanzo vya maji, aidha amewaomba viongozi wa kisiasa kufanya maamuzi magumu katika utekelezaji wa usimamizi wa kutunza mazingira na hasa kuwasihi wananchi wasilime vinyungu kando na vyanzo vya maji kwa faida ya vizazi vya sasa na vijavyo.

Kwa upande wake Mkuu wa Wilaya Mufindi Mhe Jamhuri William amesema katika utunzaji wa vyanzo vya maji tayari wako katika hatua mbalimbali za utunzaji na tayari wamebainisha zaidi ya vyanzo 1900 vya maji ndani ya Wilaya ya Mufindi ambavyo vimewekewa mkakati kabambe wa kuvitunza.

Amewaomba wananchi kuendelea kuheshimu alama zilizowekwa na maelekezo waliyopewa kwa mujibu wa sheria.
“Lakini kama tukiona haiwezekani hatutasita kuwachukuia hatua za kisheria ikiwa ni pamoja na kuwapeleka mahakamani wote wanaokiuka sheria na taratibu za utunzaji mazingira kati vyanzo vyetu vya maji” Alisema Mhe. William.

Ikumbukwe kuwa sheria ya mazingira inasema kuwa ndani ya mita 60 katika eneo la chanzo cha maji hairuhusiwi kufanya shughuli yoyote.
Nae Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya Mufindi  Mhe Festo Mgina amesema wao kama wanasiasa wanaungana na viongozi wa serikali kuendelea kutoa elimu ya mazingira kwa wananchi ili waendelee kutambua umuhimu wa utunzaji wa vyanzo vya maji.

Aidha Meneja Mkuu wa Mwenga Hydro Power chini ya Kampuni tanzu ya Rift Valley Energy Mhandisi Joel Gomba amesema wameanza kujena mitambo ya kuzalisha umeme kwa kutumia upepo ambao unatarajiwa kukamilika na kuanza kutumika mwakani ili kuongeza nguvu kwenye gridi ya Taifa na inategemewa kuzalishwa Megawati 2.4.

Kwa upande wake Meneja TANESCO Wilaya ya Mufindi Mhandisi Omary Ally akitoa taarifa ya utekelezaji wa umeme Wilaya ya Mufindi kwa Naibu Waziri wa Nishati alisema Wilaya inapokea umeme kutoka kwa mzalishaji binafsi MWENGA HYDRO POWER anaezalisha kiasi cha zaidi ya Megawati 3.5 MW na kuvisambazia umeme jumla ya vijiji 32 na wateja 2800.

TANESCO Wilaya ya Mufindi inaundwa na Halmashauri ya Mji Mafinga na Halmashauri ya Wilaya Mufindi yenye Kituo cha kupooza umeme Mgololo (220/33/11) Kv, Wilaya ina hudumia wateja wapatao 16,436 wa Halmashauri ya Mji Mafinga na Mufindi wateja wakubwa 108 wa kati 370 na wadogo 15, 958 aidha Wilaya inauwezo wa 30MW (Capacity) na matumizi ya juu ni  9.5MW Megawati.


HABARI PICHA
Naibu Waziri wa Nishati Mhe Subira Mgalu akipokelewa na Mkuu wa Wilaya Mufindi Mhe Jamhuri William

Naibu Waziri Subira Mgalu akisalimiana na Kamanda Kikosi wa Mafinga JKT Luteni Kanali D. Chalamila

Naibu Waziri Mgalu akisalimiana na Afisa Uhamiaji Wilaya ya Mufindi
Naibu Waziri wa Nishati Subira Mgalu akisalimiana na Kamanda wa Zimamoto Wilaya ya Mufindi Jackline Mtei



Naibu Waziri wa Nishati Subira Mgalu akisalimiana na Mwenyekiti wa Halmashauri ya Mji Mafinga

Naibu Waziri wa Nishati Subira Mgalu akisalimiana na Meneja TANESCO Wilaya ya Mufindi Mhandisi Omary Ally

Naibu Waziri Nishati Akisaini Kitabu katika Ofisi ya Mkuu wa Wilaya Mufindi


Naibu waziri Mgalu akieleza lengo kuu la Ziara yake Wilaya ya Mufindi


Pichani: Katikati  ni Naibu Waziri wa Nishati Subira Mgalu Kulia Kwake ni Mwenyekiti wa ccm Wilaya ya Mufindi na Kushoto kwake ni Mkuu waWilaya ya Mufindi Mhe Jamhuri William na wa mwisho kulia ni Mwenyekiti wa Halmashauri ya Mji Mafinga Mhe Charles Makoga  na Mwisho Kushoto ni Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya Mufindi Mhe Festo Mgina


Naibu waziri Subira Mgalu akiwa na Mwenyekiti wa CCM Wilaya ya Mufindi

Meneja TANESCO Wilaya Mufindi Mhandisi Omary Ally akitoa maelezo kwa Naibu Waziri wa Nishati Katika Kijiji Cha Ikongosi


Mwenyekiti wa Kijiji cha Ikongosi akitoa salamu za shukrani kwa Naibu Waziri wa Nishati Wakati wa hafla ya Uwashaji wa Umeme katika Kijiji Hicho


Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya Mufindi Mhe Festo Mgina

Mwenyekiti wa Halmashauri ya Mji Mafinga Mhe Charles Makoga


Meneja  TANESCO Kutoka Ofisi za Nyanda za Juuu Kusini


Meneja TANESCO Mufindi Mhandisi Omary Ally



Naibu Waziri wa Nishati Mhe Subira Mgalu akiongea na Wananchi wa Kijiji cha  Ikongosi wakati wa Uwashaji wa Umeme katika Kijiji hicho



Ukataji wa tepe kuashairia uwashaji wa umeme Ikongosi



Katika Ofisi ya Kijiji

Katika Ofisi za Mwenga



Meneja Uendeshaji Mwenga Hydro Power chini ya Kampuni tanzu ya Rift Valley Energy Eng. Joel Gomba



Kuelekea kwenye chanzo cha Umeme Mwenga Hydro Power 


Mwenga Hydro Power Mufindi

Eng. Joel Gomba akimuonesha Naibu Waziri wa Nishati hatua za uzalishaji umeme kwa njia ya maji katika chanzo cha umeme Mwenga







Naibu Waziri wa Nishati Subira Mgalu akifurahia chanzo cha umeme wa nguvu ya Maji Mwenga

Naibu Waziri Nishati Subira Mgalu
Amani Mbwaga



Kulia nia Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya Mufindi  Mhe festo Mgina na Kushoto ni Mwenyekiti wa Halmashauri ya Mji Mafinga Mhe Charles Makoga wakiwa katika Chanzo cha Umeme Mwenga





Baadhi ya Mitambo



Naibu Waziri Nishati akikagua Mitambo ya uzalishaji Umeme


(Picha zote na Amani Mbwaga)
Kwa Maoni Au Ushauri Wasiliana nasi:
Mob:+255 656 632 566
E-mail:prof.mbwaga@gmail.com
Twitter:@amanimbwaga