Sunday, November 11, 2018

IHALIMBA MISITU FC NA IHEFU MISITU FC ZATINGA FAINALI

Na Amani Mbwaga, Mafinga,

Ihalimba Misitu FC
Ni katika mashindano ya Misitu Sports Bonanza yanayodhaminiwa na Wakala wa huduma za Misitu Tanzania (TFS) Shamba la miti Sao Hill ambayo yalifikiwa hatua ya nusu fainali iliyopigwa jana jumapili baada ya kuzikutanisha timu za Tarafa ya Kwanza hadi ya nne ambazo ni Ihalimba Misitu FC Vs Villa FC na Ihefu Misitu Vs Sawala FC.Katika mtanange wa kwanza ulizikutanisha Ihalimba Misitu Fc dhidi ya Villa Fc Ihalimba iliweza kuichabanga Villa Fc Mabao 4-1 Magoi yaliyofungwa na Zackaria, Melick, Issa na Stanley Wakati bao la kufutia machozi la Villa FC likifungwa na Joshua Kadinda.


Mchezo wa Pili ulizikutanisha timu za Ihefu Misitu Fc dhidi ya Sawala Fc mchezo huu uligubikwa na bonge la mvua mwanza wa mchezo hadi mwisho lakini pira uliendelea mpaka kipyenga cha mwisho kinapigwa Ihefu Misitu FC iliweza kuchomoza na ushindi wa mabao 2-0 amaao sawala hawakupata kitu mbali ya hapo waliambulia kadi nyekundu kwa beki wao mahili ajulikanae kwa jina la Tenende.
Hivyo basi kwa mujibu wa Mwenyekiti wa Mshindano hayo ya Misitu Bonanza Shamba la Miti Sao Hill Bwana Saidi Aboubakar Amethibitisha kwamba Fainali ya mashindano hayo itapigwa siku ya Jumamosi ya Tarehe 17 Novema 2018 katika viwanja vya Misitu Makao makuu ya Shamba la Miti Sao Hill ambapo itazikutanisha timu za IHEFU MISITU FC kutoka Tarafa ya II Ihefu dhidi ya IHALIMBA FC kutoka Tarafa ya III na Mshindi atajinyakulia zawadi nono sana!
Aidha Bwana Said amewaomba wananchi wengi na wapenzi wa michezo kuweza kujitokeza kwa wingi kuja kushuhudia mtanange huo wa kukata na shoka, kwani siku hiyo mtoto hatumwi dukani.
Mashindano haya yamekuja kwa lengo la kuendelea kutoa elimu juu ya matumizi sahii ya moto dhidi ya mazingira na athari za uchomaji misitu, lakinin pia kuendelea kujenga mahusiano mazuri baina ya Shamba la Mti Sao Hill na Wananchi wanaolizunguka sanjari na Kurudisha shukrani kwa jamii (Corporate Social Responsibility)

HABARI PICHA
Ihalimba Misitu FC
Ihefu Misitu FC
Sawala FC





Villa FC



Meneja wa Shamba la Miti Sao Hill wa Pili Kushoto  Bwana Haule akifuatilia kwa makini mtanange wa nusu fainali wa Misitu Sports Bonanza wa kwanza kulia ni Mwenyekiti wa Mashindano hayo na Afisa Nyuki wa Shamba la Miti Sao Hill Bwana Said Aboubakar wakiwa na viongozi wengine wa TFS Sao Hill



Mechi kati ya Ihefu Fc na Sawala Fc ikiendelea wakati mvua inanyesha

Ihefu Fc
Sawala Fc

Picha zote na Amani Mbwaga
Kwa Maoni au ushauri wasiliana nasi;
Mob:+255 656 632 566
E-mail:prof.mbwaga@gmail.com

No comments:

Post a Comment