Monday, November 26, 2018

NAIBU WAZIRI WA NISHATI SUBIRA MGALU AFANYA ZIARA YA KUTEMBELEA CHANZO CHA UMEME MWENGA MIN HYDRO POWER NA KUWASHA UMEME IKONGOSI-MUFINDI.


Na Amani Mbwaga.
Naibu Waziri wa Nishati, Subira Mgalu amewasha umeme katika kijiji cha Ikongosi na Kufanya ziara ya kutembelea chanzo cha Umeme kutoka kwa Mzalishaji binafsi MWENGA HDRO POWER Chini ya Kampuni tanzu ya RIFT VALLEY ENERGY iliyopo wilayani Mufindi Mkoani Iringa.

“Nimefurahi kufika Mwenga hapa na nadhani ni mradi wangu wa kwanza kufika katika mradi kama huu wa sekta binafsi  tangu nimeteuliwa kuwa naibu waziri wa Nishati katika uzalishaji huu wa umeme kwa kutumia maporomoko ya maji, nawapongeza sana Mwenga”. anasema Mhe Mgalu

Katika suala la uhifadhi mazingira Mhe Mgalu ameitaka kamati ya ulinzi na usalama ya wilaya ya Mufindi kuchukua hatua za makusudi ili kuhakikisha vyanzo vya maji ikiwemo chanzo cha mto mwenga vinatunzwa ipasavyo ili kuwa na umeme wa uhakika na wale wanaofanya shughuli za kilimo karibu na vyanzo vya maji waondolewe mara moja bila kuoneana haya.

“Tupo katika vita ya kuhakikisha miradi inayozalishwa kwa kutumia umeme inafanya kazi kama ilivyokusudiwa, nashukuru mungu mwaka huu hatujaona athari katika Mtera na Kidatu” alisema Mhe Mgalu.

Akitoa wito kwa wakazi wa maeneo ya chanzo cha umeme wa maji Mwenga, amewataka wananchi  kuendelea kutii maagizo ya serikali za mitaa ya kutunza vyanzo vya maji, aidha amewaomba viongozi wa kisiasa kufanya maamuzi magumu katika utekelezaji wa usimamizi wa kutunza mazingira na hasa kuwasihi wananchi wasilime vinyungu kando na vyanzo vya maji kwa faida ya vizazi vya sasa na vijavyo.

Kwa upande wake Mkuu wa Wilaya Mufindi Mhe Jamhuri William amesema katika utunzaji wa vyanzo vya maji tayari wako katika hatua mbalimbali za utunzaji na tayari wamebainisha zaidi ya vyanzo 1900 vya maji ndani ya Wilaya ya Mufindi ambavyo vimewekewa mkakati kabambe wa kuvitunza.

Amewaomba wananchi kuendelea kuheshimu alama zilizowekwa na maelekezo waliyopewa kwa mujibu wa sheria.
“Lakini kama tukiona haiwezekani hatutasita kuwachukuia hatua za kisheria ikiwa ni pamoja na kuwapeleka mahakamani wote wanaokiuka sheria na taratibu za utunzaji mazingira kati vyanzo vyetu vya maji” Alisema Mhe. William.

Ikumbukwe kuwa sheria ya mazingira inasema kuwa ndani ya mita 60 katika eneo la chanzo cha maji hairuhusiwi kufanya shughuli yoyote.
Nae Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya Mufindi  Mhe Festo Mgina amesema wao kama wanasiasa wanaungana na viongozi wa serikali kuendelea kutoa elimu ya mazingira kwa wananchi ili waendelee kutambua umuhimu wa utunzaji wa vyanzo vya maji.

Aidha Meneja Mkuu wa Mwenga Hydro Power chini ya Kampuni tanzu ya Rift Valley Energy Mhandisi Joel Gomba amesema wameanza kujena mitambo ya kuzalisha umeme kwa kutumia upepo ambao unatarajiwa kukamilika na kuanza kutumika mwakani ili kuongeza nguvu kwenye gridi ya Taifa na inategemewa kuzalishwa Megawati 2.4.

Kwa upande wake Meneja TANESCO Wilaya ya Mufindi Mhandisi Omary Ally akitoa taarifa ya utekelezaji wa umeme Wilaya ya Mufindi kwa Naibu Waziri wa Nishati alisema Wilaya inapokea umeme kutoka kwa mzalishaji binafsi MWENGA HYDRO POWER anaezalisha kiasi cha zaidi ya Megawati 3.5 MW na kuvisambazia umeme jumla ya vijiji 32 na wateja 2800.

TANESCO Wilaya ya Mufindi inaundwa na Halmashauri ya Mji Mafinga na Halmashauri ya Wilaya Mufindi yenye Kituo cha kupooza umeme Mgololo (220/33/11) Kv, Wilaya ina hudumia wateja wapatao 16,436 wa Halmashauri ya Mji Mafinga na Mufindi wateja wakubwa 108 wa kati 370 na wadogo 15, 958 aidha Wilaya inauwezo wa 30MW (Capacity) na matumizi ya juu ni  9.5MW Megawati.


HABARI PICHA
Naibu Waziri wa Nishati Mhe Subira Mgalu akipokelewa na Mkuu wa Wilaya Mufindi Mhe Jamhuri William

Naibu Waziri Subira Mgalu akisalimiana na Kamanda Kikosi wa Mafinga JKT Luteni Kanali D. Chalamila

Naibu Waziri Mgalu akisalimiana na Afisa Uhamiaji Wilaya ya Mufindi
Naibu Waziri wa Nishati Subira Mgalu akisalimiana na Kamanda wa Zimamoto Wilaya ya Mufindi Jackline Mtei



Naibu Waziri wa Nishati Subira Mgalu akisalimiana na Mwenyekiti wa Halmashauri ya Mji Mafinga

Naibu Waziri wa Nishati Subira Mgalu akisalimiana na Meneja TANESCO Wilaya ya Mufindi Mhandisi Omary Ally

Naibu Waziri Nishati Akisaini Kitabu katika Ofisi ya Mkuu wa Wilaya Mufindi


Naibu waziri Mgalu akieleza lengo kuu la Ziara yake Wilaya ya Mufindi


Pichani: Katikati  ni Naibu Waziri wa Nishati Subira Mgalu Kulia Kwake ni Mwenyekiti wa ccm Wilaya ya Mufindi na Kushoto kwake ni Mkuu waWilaya ya Mufindi Mhe Jamhuri William na wa mwisho kulia ni Mwenyekiti wa Halmashauri ya Mji Mafinga Mhe Charles Makoga  na Mwisho Kushoto ni Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya Mufindi Mhe Festo Mgina


Naibu waziri Subira Mgalu akiwa na Mwenyekiti wa CCM Wilaya ya Mufindi

Meneja TANESCO Wilaya Mufindi Mhandisi Omary Ally akitoa maelezo kwa Naibu Waziri wa Nishati Katika Kijiji Cha Ikongosi


Mwenyekiti wa Kijiji cha Ikongosi akitoa salamu za shukrani kwa Naibu Waziri wa Nishati Wakati wa hafla ya Uwashaji wa Umeme katika Kijiji Hicho


Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya Mufindi Mhe Festo Mgina

Mwenyekiti wa Halmashauri ya Mji Mafinga Mhe Charles Makoga


Meneja  TANESCO Kutoka Ofisi za Nyanda za Juuu Kusini


Meneja TANESCO Mufindi Mhandisi Omary Ally



Naibu Waziri wa Nishati Mhe Subira Mgalu akiongea na Wananchi wa Kijiji cha  Ikongosi wakati wa Uwashaji wa Umeme katika Kijiji hicho



Ukataji wa tepe kuashairia uwashaji wa umeme Ikongosi



Katika Ofisi ya Kijiji

Katika Ofisi za Mwenga



Meneja Uendeshaji Mwenga Hydro Power chini ya Kampuni tanzu ya Rift Valley Energy Eng. Joel Gomba



Kuelekea kwenye chanzo cha Umeme Mwenga Hydro Power 


Mwenga Hydro Power Mufindi

Eng. Joel Gomba akimuonesha Naibu Waziri wa Nishati hatua za uzalishaji umeme kwa njia ya maji katika chanzo cha umeme Mwenga







Naibu Waziri wa Nishati Subira Mgalu akifurahia chanzo cha umeme wa nguvu ya Maji Mwenga

Naibu Waziri Nishati Subira Mgalu
Amani Mbwaga



Kulia nia Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya Mufindi  Mhe festo Mgina na Kushoto ni Mwenyekiti wa Halmashauri ya Mji Mafinga Mhe Charles Makoga wakiwa katika Chanzo cha Umeme Mwenga





Baadhi ya Mitambo



Naibu Waziri Nishati akikagua Mitambo ya uzalishaji Umeme


(Picha zote na Amani Mbwaga)
Kwa Maoni Au Ushauri Wasiliana nasi:
Mob:+255 656 632 566
E-mail:prof.mbwaga@gmail.com
Twitter:@amanimbwaga

No comments:

Post a Comment