Saturday, November 3, 2018

Misitu Sports Bonanza Imeendelea Kutimua Vumbi leo katika viwanja vya Misitu Sao Hill Mjini Mafinga.

Na Amani Mbwaga, Mufindi.
Ihefu Fc Mabingwa Tarafa ya II Ihefu
Mashindano ya Mpira wa miguu ya Misitu Sports Bonanza Chini ya Udhamini mkuu wa Wakala wa huduma za  Tanzania (TFS) Shamba la Misitu Sao-Hill yameendelea kutimua vumbi mapema leo hii katika viwanja vya Misitu Sao Hill vilivyopo ndani ya tarafa ya pili Ihefu Wilayani Mufindi Mkoani Iringa.

Mashindano hayo yameshirikisha timu 8 kutoka katika vijiji mbalimbali vinavyozunguka shamba la miti Sao-Hill Kundi A ilishirikisha timu za Matanana FC, Mtula FC, Sao Hill FC na Bumilayinga FC Kundi  B ni TWICO FC, Ihefu FC, Changarawe FC na Nyororo FC.

Timu ya IHEFU FC imefanikiwa kutwaa ubingwa kwa ushindi mabao 2-0 dhidi ya SAO HILL FC Magoli yote yamefungwa na mshambuliaji hatari EDWINI ILOMO timu hiyo sasa inaiwakilisha Tarafa ya pili ya Ihefu  kuelekea  hatua ya nusu fainali.

Aidha Mshindi wa kwanza amepewa zawadi ya Pea moja ya jezi na mshindi wa pili amepewa zawadi ya mpira mmoja.
Mgeni wa Heshima wa bonanza hilo alikuwa Meneja wa Shamba la Miti Sao Hill Bwana Heriberth Haule.

Mashindano haya ya bonanza yanalengo la kukumbusha jamii kuhusu matumizi bora ya moto hasa wakati huu wa maandalizi ya mashamba ili kuepuka hasara inayoweza kujitokeza kwa kuunguza misitu ya serikali na watu binafsi lakini vileveile kutoa elimu ya ufugaji nyuki na kuendeleza mahusiano mazuri baina ya Shamba na Jamii inyozunguka.

 Bonanza hili litaendelea katika Tarafa ya Shamba la Misitu Sao Hill , Irundi ambapo mshindi wa kesho nae atapata zawadi ya jezi na baade kuingia hatua ya nusu fainali.  


Shamba la miti Sao Hill lina dira ya kuwa na misitu iliyojifadhiwa ikiwa na matumizi endelevu na kulinda kwa kushirikisha jamii.

HABARI PICHA


Mgeni wa Heshima Meneja wa Shamba la Miti Sao Hill Bwana Herberth Haule akimkabidhi zawadi Mshindi wa Pili wa Tarafa ya Pili ya Ihefu timu ya Sao Hill Kijiji

Timu ya Sao Hill Kijiji FC

Mgeni wa Heshima Meneja wa Shamba la Miti Sao Hill Bwana Herberth Haule akimkabidhi zawadi Mshindi wa Kwanza wa Tarafa ya Pili ya Ihefu timu ya Ihefu FC

Timu ya Ihefu FC Washindi wa kwanza wa Tarafa ya II ya Ihefu













 



Washabiki wa timu ya Ihefu FC Wakifurahia ushindi baada ya timu yao kuchukua nafasi ya ushindi wa kwanza.
Picha zote na Amani Mbwaga

No comments:

Post a Comment