Wednesday, November 14, 2018

Mwenyekiti wa Halmashauri ya Mji Mafinga Aoongoza Songambele ya Ukarabati wa Madarasa Shule ya Msingi Mamba na Kuokoa zaidi ya Milioni 4.


Na Amani Mbwaga, Mafinga.
Mwenyekiti wa Halmashauri ya Mji Mafinga Mhe Charles Makoga leo ameongoza wananchi katika shughuli za maendeleo ya kijiji cha Isalavanu katika ukarabati wa Shule ya Msingi Mamba iliyoko katika Kata ya Isalavanu Halmashauri ya Mji Mafinga M`koani Iringa.

Zaidi ya Milioni 4 zimeokolewa kwa siku moja kutokana na nguvu za Wananchi, Mchango wa Mhe Charles Makoga akishusha Mifuko 60 ya Cement yenye thamani ya Tsh 900,000/= na Mdau wa Maendeleo ambae ni Mkurugenzi wa Kituo cha Afya Tumain Jipya Dkt. Basil Tweve ambae amechangia vifaa vyenye thamani ya zaidi ya Milioni 4.

Mhe Makoga amewapongeza wananchi kwa kujitokeza kwa wingi katika zoezi hilo ambapo zaidi ya wananchi 300 wa kijiji cha Isalavanu wameshiriki katika ujenzi huo na kumtaka Afisa mtendaji wakijiji kuthaminisha nguvu ya wananchi kama Rais Dkt John Pombe Magufuli anavyotaka nguvu ya wananchi ithaminishwe na isomwe kwenye taarifa za mapato na matumizi ya kijiji na Shule hii ndio aliyoisoma Mhe Makoga.

“Wananchi ninawapongeza kwa mwitilio wenu na mmejenga wenyewe kwa nguvu zenu, naomba tumalizie jengo hili na tutahakikisha majengo yote yanapakwa rangi na tayari nimeshamwagiza Afisa Mipango Miji aje afanye tathimini hapa ya kazi iliyobakia ili serikali iweze kuwaletea fedha kama Milioni 10 hivi kwa sababau tayari mmeonesha nia” alisema Mhe Makoga  

Akisoma taarifa ya utekelezaji wa ujenzi huo kwa wananchi Afisa Mtendaji wa Kijiji cha Isalavanu Bwana Noel Kabinda alisema wanachi wamejitokeza kwa wingi kutokana na uhamasishaji uliofanywa na Mhe Mwenyekiti wa Halmashauri yaMji Mafinga ambae ndie diwani wa kata hiyo ya Isalavanu, kutokanana na Mahafali ya darasa la saba lilipoibuka suala la ukarabati wa shule hiyo kupitia kwa aliyekuwa mgeni rasmi Dkt Basil Tweve.

Jumla ya vyumba 02 vya madarasa ofisi 01 ya waalimu, Jiko la Muda la Kupikia chakula cha wanafunzi shuleni, ujenzi wa vyoo vya wanafunzi vyenye matundu 14 vimekarabatiwa kwa siku moja, aidha oparesheni ondoa nyasi kwenye nyumba za waalimu imefanyika ili kuweka mazingira mazuri ya kuishi kwa waalimu wa shule hiyo.

Akitoa shukrani za pongezi kwa niaba ya Wananchi Mmoja wa wakazi wa kijiji cha Isalavanu ambae pia ni katibu wa Chama cha demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) katika Kata hiyo Bwana Fulgence Kadinde ambae pia alisoma shule hiyo toka mwaka 1981 hadi mwaka 1987 ameishukuru serikali chini ya Mhe Makoga kwa kushirikiana  kuhamasisha wananchi katika shughuli hizo za maendeleo.

“Maendeleo hayana chama  kwani leo wote tupo hapa bila kujali vyama vyetu katika shughuli za kuleta maendeleo yetu hasa katika ujenzi wa shule yetu hii ya msingi Mamba, nakupongeza kwa kutafuta wadau lakini pia ongeza badii ya kiutendaji na katika hili tunakusifu na tunakupenda sana maneno ya kisiasa tuyafunike endelea kupiga kazi” alisema Ndugu Kadinde

Kwa upande wake mmoja wa waalimu wakongwe na waanzilishi wa shule hiyo toka inafunguliwa rasmi mwaka 1977 akiwa Mwalimu Mkuu Msaidizi Mwl. Leonya Victory Kalinga amesema toka shule hiyo inaanzishwa hajawahi kuona mwitikio mkubwa wa wananchi katika shughuli za maendeleo ya ujenzi wa shule hiyo imekuwa historia kubwa katika kijiji hicho kuwahi kutokea.

Shule ya Msingi Mamba ilianzishwa rasmi mnamo tarehe 07 Novemba 1977 chini ya Mwalimu Mkuu wa Kwanza Mwl. Joseph Mbishi na inamilikiwa na Halmashauri ya Mji Mafinga Mkoani Iringa na ndio shule aliyoisoma Mwenyekiti wa Halmashauri ya Mji Mafinga Mhe. Charles Makoga toka darasa la kwanza hadi hadi la saba.

HABARI PICHA








































No comments:

Post a Comment