Tuesday, September 19, 2017

Vijana wanaopitia JKT hufanikiwa katika Maisha.


Na Amani Mbwaga                                                15 Septemba 2017 Mafinga, Tanzania.
Mgeni Rasmi Mkuu wa Mkoa Mhe.Amina Masenza akikagua gwaride la vijana Mujibu wa Sheria Op Tanzania ya Viwanda 2017 katika kikosi cha Jeshi Mafinga JKT.
 (Picha na Amani Mbwaga)
Hayo yamesemwa na Mkuu wa Mkoa Iringa Mhe Amina Juma Masenza wakati wa Kufunga Mafunzo ya awali ya Kijeshi kwa Vijana wa JKT Mujibu wa Sheria kundi Tanzania ya Viwanda katika Kikosi cha Jeshi la Kujenga Taifa Mafinga (JKT)  kilichopo Wilaya ya Mufindi Mkoani Iringa.

“Uzoefu unaonesha kuwa vijana wote wanaopita JKT hufanikiwa katika Maisha yao kutokana na kuwaandaa vijana kuwa na Uzalendo Uadilifu Ukakamavu, Utii, Uhodari, Uaminifu na kwa kujifunza shughuli mbalimbali za uzalishaji mali” alisema Mhe Masenza.

Pamoja na kwamba JKT halitoi ajira kwa vijana lakini mafunzo haya waliyoyapata ni sawa na ajira, kwani wamejifunza, Kilimo Ufugaji, utunzaji wa mazingira na shughuli nyingine za mikono, hizo ni fursa za ajira zitakazowafanya waweze kujitegemea katika hali yoyote.

Aidha Mhe Masenza alitoa wito kwa vijana wahitimu kwamba mafunzo ya Kijeshi waliyoyapata yakaimarishe amani na utulivu wa nchi na jamii kwa ujumla.

Pia amewataka vijana wakadumishe sifa nzuri ya Mafinga JKT na Jeshi kwa Ujumla.

Naye Mwakilishi wa Mkuu wa JKT Meja Jenerali Michael Isamuhyo na Mkurugenzi wa ustawi wa Jamii JKT Kaimu Kanali AS Kagombola alisema mafunzo hayo ya Jeshi la Kujenga Taifa  yamelenga kuwaanda vijana wa Kitanzania kuwa na moyo wa Uzalendo, Kupenda kazi za Mikono Kujituma, Kuilinda, Kuitetea na Kuifia nchi yao.

Aidha katika kutekeleza majukumu makuu ya JKT Uzalishaji Mali, Mafunzo ya awali ya Kijeshi na Malezi kwa vijana ikiwemo stadi za maisha na stadi za kazi kuwa kielelezo cha kutosha kwa jamii.

Pamoja na majukumu yote hayo JKT imeendelea kuboresha miundombinu ya Vikosi mbalimbali vya Jeshi ili kuweza kuongeza idadi kubwa ya Vijana kujiunga na Mafunzo hayo muhimu kwa Taifa

Kwa upande wake Mkuu wa Kikosi cha Mafinga JKT Luteni Kanali Hamisi Maiga aliwataka vijana kutoyumbishwa na watu wasiolitakia mema taifa letu bali wazingatie kiapo chao cha Utii, Uhodari na Uaminifu
“Fanyeni mambo yenye tija kwa taifa na yasiyo na tija achaneni nayo” alisema Luteni Kanali Hamisi Maiga

Waasisi wa Taifa letu waliona umuhimu wa vijana wa kitanzania kupata mafunzo na kutoa malezi kwa lengo la kutetea na kulilinda taifa ili kuendana na mila na desturi na utamaduni wa Taifa letu .

JKT ilipewa jukumu la malezi kwa vijana kwa lengo la kuondoa  makovu yaliyoachwa na wakoloni ambayo yalianza kuenezwa kwa vijana wasomi kwa wakati huo.

Kabla ya kuanzishwa chombo hiki vijana wale wasomi walijengewa kasumba ya wao kuwa bora kuliko vijana wengine  waliopata elimu ya kiwango cha chini, hali hii ilipelekea mgawanyiko wa matabaka ya kielimu.

Kwa kuona umuhimu huo JKT Ilianzishwa rasmi na kuanza kutoa Mafunzo ya vijana wasomi na wasiosoma bila kubaguana, baadae JKT iliongezewa jukumu la uzalishaji mali na Ulinzi.

JKT ilianzishwa Julai 10, 1963 katika uwanja wa ndani wa michezo wa Taifa (Indoor Stadium) majira ya saa kumi na moja jioni, ambapo vijana 11 kutoka wilaya 11 wakiwa makatibu wa vijana TYL walijiunga kwa mafunzo katika kambi ya JKT Mgulani jijini Dar es salaam

Sanjari na hilo Mwaka 1964 ilitungwa Sheria ya JKT (The National Service Act) ambayo ilimpa madaraka Mkurugenzi wa JKT Kuandikisha Vijana wa Kujitolea Kujiunga na Jeshi la Kujenga Taifa.

Sheria hiyo ilifanyiwa marekebisho mwaka 1966 na 1967 ili kuwawezesha vijana waliokuwa wakihitimu elimu ya Sekondari ya Kidato cha nne na Sita Kujiunga JKT Kwa mujibu wa Sheria.

Mafunzo haya ya JKT kwa vijana wa Kujitolea na Mujibu wa sheria yaliendelea kwa ufanisi mpaka mwaka 1994, serikali ilipositisha kwa sababu mbalimbali za Kiuchumi.

Kusitishwa kwake, watafiti walisema kuwa jamii ilishuhudia mmomonyoko mkubwa wa maadili na uwajibikaji usiozingatia nidhamu, hasa kada ya vijana.

Mmomonyoko huo ulizusha malalamiko ya makundi mbalimbali ya jamii yakitaka kurejeshwa kwa taasisi hiyo, hali iiyowezeshwa na Serikali ya Awamu ya Tatu chini ya Rais na Amiri Jeshi Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe Benjamini William Mkapa, Kuyahuisha Mwaka 2001 kwa Vijana wa Kujitolea .

Mnamo machi 26 mwaka 2013, Serikali ya Awamu ya nne chini ya Amiri Jeshi  Mkuu na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt Jakaya Mrisho Kikwete alizindua upya mpango wa Mafunzo ya JKT kwa vijana wa Mujibu wa Sheria.

Hadi sasa katika Serikali hii ya awamu ya tano ya Rais na Amiri Jeshi Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe Dkt John Pombe Magufuli imeendelea kutoa mafunzo hayo ya vijana wa mujibu wa Sheria na Kujitolea kwa Kiwango cha hali ya juu hii inatokana na kurejeshwa kwa baadhi ya Makambi ya JKT yakiwemo ya Makuyuni, Mpwapwa, Itaka, Milundikwa, na Luwa.


Mgeni Rasmi na Mkuu wa Mkoa wa Iringa Mhe Amina Juma Masenza akipokea Salamu ya heshima kutoka katika gwaride la vijana Mujibu wa sheria Op Tanzania ya Viwanda 2017 katika kikosi cha Jeshi Mafinga (Picha Na Amanin Mbwaga)










Baadhi ya  ndugu, jamaaa na wananchi wa mji wa Mafinga wakifuatilia kwa makini Paredi ya Vijana wa JKT Mafinga

Kijana wa JKT Mujibu wa Sheria Service Man Mshindi wa Kwata akipokea zawadi

Kijana wa JKT  Service Girl Mshindi wa Usafi akipokea zawadi

Paredi Ikitoka nje ya Uwanja





Kikundi cha Kwaya ya Vijana Wa JKT Mujibu wa Sheria 2017 


Kikundi cha Ngoma cha Mafinga JKT






Kikundi cha Sarakasi cha Mafinga JKT






Kikundi cha Singe cha Vijana Mujibu wa Sheria OP Tanzania ya Viwanda Mfinga JKT 2017


Kikundi cha Kareti Op Tanzania ya Viwanda Mujibu wa Sheria 2017





Vijana wa JKT Mafinga wakionesha uwezo wao Mkubwa wa Kareti


Mgeni Rasmi Mkuu wa Mkoa wa Iringa Mhe Amina Juma Masenza akimshukuru  Afisa Habari na Uhusiano wa Mafinga JKT Koplo Elias Mbega mara baada ya Kukabidhiwa zawadi iliyoandaliwa na Ofisi ya Habari na Uhusiano Mafinga JKT (Picha na Amani Mbwaga)



Kijana wa wa Kikundi cha Sanaa Mafinga JKT Service Man Paul Kwayu akimkabidhi Mkuu wa Kikosi Luteni Kanali Hamis Maiga CD ya Kwaya ya Kikosi Mafinga JKT.
Mkuu wa Mkoa wa Iringa Mhe Amina Juma Masenza akihutubia Hadhara iliyojitokeza katika Mahafali ya Vijana wa Mujibu wa Sheria Op Tanzania ya Viwanda 2017
Mwakilishi wa Mkuu wa JKT na Mkurugenzi wa Ustawi wa Jamii JKT Kaimu Kanali AS Kagombola kitoa Salamu za  Mkuu wa JKT

Kamanda Mkuu wa Kikosi cha Mafinga JKT Luteni Kanali Hamis Maiga akiwaasa Vijana wa JKT


Mgeni rasmi akiwa katika Picha ya Pamoja na aadhin ya Maofisa na askari wa  Kikosi cha Jeshi Mafinga


Mkuu wa Mkoa akia katika Picha ya Pamoja na viongozi wa Vijana OP Tanzania ya Viwanda 2017 (Picha zote na Amani Mbwaga)


Kwa mawasiliano zaidi Wasiliana nasi:
Mob 0765058711
        0656632566
Email:prof.mbwaga@gmail.com