Tuesday, July 16, 2019

Waziri wa Viwanda na Biashara na Mbunge wa Karagwe Mhe. Bashungwa azind...

Waziri Bashungwa Azindua ligi ya Mpira wa Miguu Karagwe


Na Amani Mbwaga,  Karagwe

Waziri wa Viwanda na Biashara ambae pia ni Mbunge wa Jimbo la Karagwe Mkoani Kagera Mhe. Innocent Bashungwa Mapema Wikendi iliyopita amezindua rasmi Mashindano ya ligi ya mpira wa miguu ambayo hufanyika kila mwaka Jimboni kwake na ni maarufu kwa BASHUNGWA KARAGWE CUP.

Akiongea na Wananchi katika kijiji cha Nyakagoyagoye Wilayani Karagwe wakati wa uzinduzi wa ligi hiyo Waziri Bashungwa amesema  wananchi wanapoendelea kuchapa kazi serikali nayo inaendelea kuleta huduma za jamii katika maeneo yote mijini na vijijini.

“Wana Karagwe Chapeni Kazi lakini sisi kwenye huduma za jamii suala la maji mlikuwa mkisikia nikiwa bungeni nazungumzia mradi wa maji mpaka koo linakauka, lakini huo mradi ndugu zangu ni mkubwa sana na uko katika hatua nzuri na hivi ninavyozungumza Waziri wa maji alikuwa hapa Karagwe jana kuhakikisha mradi huo unatekelezwa ipasavyo” alisema

Wakati huo huo Waziri Bashungwa amemshukuru Rais Magufuli kwa kupeleka miradi mingi na mikubwa Wilayani Karagwe ambapo hivi  karibuni tu Zaidi ya Bilioni 70 zitapelekwa tena katika Wilaya hiyo kwa ajili ya kuchochea miradi mingine ya maendeleo.

Mkuu wa Wilaya Karagwe Mhe. Godfrey Mhehuka amempongeza waziri Bashungwa kwa kuchapa kazi na hatimae wana karagwe wanafurahia maendeleo yanayopatikana ktokana na juhudi zake.
“Niemona niseme pongezi zangu kwako, umati huu ni mkubwa sana na unaona ni kwa sababu wewe umeamua kufanya kitu.

Aidha. Mhe Mheuka ameendelea kusema rais hakukosea kumchagua kuwa waziri wa viwanda na biashara hivyo amemuomba akachape kazi na wao wako nyuma yake kuhakikisha anawatumikia vyema wananchi wa Karagwe na Taifa kwa ujumla.

“Niseme neno moja tu, Mungu ametuona, nataka niwape siri hakika mungu amewaona DC Mwenye Waziri Mkoa wa Kagera niko peke yangu ahsanteni sana”alisema Mhe. Mheuka

Kwa mujibu wa mratibu wa mashindano ya BASHUNGWA KARAGWE CUP Bwana Majaliwa Said amesema  Mashindano hayo yameanza tarehe 13 Julai 2019 yakihusisha timu kutoka kata zote 23 za Halmashauri ya Wilaya Karagwe.

Jiogarafia ya karagwe ni kubwa hivyo tumetengeneza kanda mbalimbali ambazo zitakuwa  zinashindana na baadae kuingia katiak 16 bora hadi fainali
HABARI PICHA

Waziri wa Viwanda na Biashara Mhe.Innocent Bashungwa (Kushoto) akifurahia jambo na Mkuu wa Wilaya Karagwe Mhe.Godgrey Mhehuka katikati ni Katibu wa CCM wilaya ya Karagwe Bi. Mary Kananda
Pichani, Waziri wa Viwanda na Biashara Mhe. Innocent Bashungwa wa (tatu kushoto) akiwa pamoja na moja ya Timu iliyozindua mchezo wa kwanza wa ligi ya Bashungwa Karagwe Cup





Waamuzi na Ma Kapteni wa Timu

Baadhi ya Wananchi waliofika Kuhudhuria Uzinduzi wa Bashungwa Karagwe Cup Wkifuatilia kwa Makini Mchezo unaoendelea

Mratibu wa Mashindano ya BASHUNGWA KARAGWE CUP Bwana Majaliwa Said akitoa Taarifa ya Mashindano kwa Waziri wa Viwanda na Biashara  (Mbunge Karagwe) 



Wawakilishi wa Timu mbalimbali kutoka katika Kata 23 za Halmashauri ya Wilaya Karagwe wakifurahia Vifaa vya jezi na mipira vulivyotolewa na Waziri Bashungwa  wakati wa Uzinduzi wa Mashindano hayo. (Picha zote na Amani Mbwaga)

Friday, July 5, 2019

Waziri wa Viwanda na Biashara Mhe. Bashungwa Afanya ziara katika Viwanda vya nguo na Kutatua kero zao


Na Amani Mbwaga, Dar es salaam
Waziri wa viwanda na Biashara nchini Tanzania Mhe. Innocent Bashungwa Mapema leo hii amefanya ziara katika viwanda vya nguo kikiwemo cha NIDA na kile cha NAMERA vya jijini Dar es salaam.

Akiongea mara baada ya kutembelea viwanda hivyo Mhe. Bashungwa amesema lengo la ziara hiyo ni kupita katika viwanda vyote vya nguo nchini kujua changamoto zao na kisha serikali kuzifanyia kazi na hatimae kuwa na uzalishaji endelevu wa zao la  pamba na kuwanufaisha wakulima.

“Mimi nimekuja hapa kwa ziara mahususi, Wakulima wetu wa pamba wamehamasika sana kulima pamba, Msimu huu wa mwaka 2019 tunategemea kuvuna  zaidi ya Tani Laki 4 za pamba  kutoka tani Laki 220,000 za mwaka jana kwa hiyo tuna pamba za kutosha” alisema  Mhe. Bashungwa.

Aidha amesisitiza kwamba wakulima kwa upande wao wametimiza wajibu wao hivyo ni jukumu la Serikali kupitia wizara ya viwanda na biashara kuwatafutia masoko yenye tija.

“Kwa muda mrefu soko la pamba limekuwa likitegemea mlango mmoja tu, wakati wa enzi za Baba wa Taifa Mwl. Julius Nyerere kulikuwa na viwanda vingi vya nguo na vilikuwa vinafanya kazi ipasavyo na kama vyote vingekuwepo basi kusingekuwepo na changamoto ya masoko katika zao la pamba hivyo ni wakati sasa wa viwanda vilivyopo na vitakavyojengwa kuhakikisha vinafanya kazi ipasavyo na Kuongeza Uzalishaji mara mbili zaidi  ili kuendana na kasi ya sasa ya Tanzania ya Viwanda".

Nchi ikifanikiwa kuchakata kila zao na kuliongezea thamani basi itakua ni chachu ya ongezeko la ajira hapa nchini na hatimae kukuza uchumi wa  taifa na wananchi kwa ujumla.

Dira kuu ya Wizara ya Viwanda na Biashara  ni "Kuwa na msingi shindani wa viwanda, mazingira bora ya uwekezaji na ukuaji wa biashara unaowezesha kukua kwa uchumi shirikishi na endelevu."

Waziri Bashungwa ataendelea na ziara hiyo nchi nzima baada ya Kuanza na Mkoa wa Kilimanjaro hapo jana na leo hapa Jijini Dar es salaam.


MATUKIO KATIKA PICHA
Waziri wa Viwanda na Biashara Mhe. Innocent Bashungwa akiangalia Bidhaa zinazotengenezwa na Kiwanda cha Nguo NIDA Wakati wa ziara yake.
Mhe.Waziri Bashungwa wakati wa Majumuisho ya ziara

Pamba ikiwa katika Hatua za awali za uchakataji

Waziri wa Viwanda na Biashara (Katikati) akipokea maelezo ya namna Pamba inavyoanza kuchakatwa katika hatua za awali




Shughuli za Uzalishaji Kiwandani zikiendelea






Waziri wa Viwanda na Biashara Mhe. Innocent Bashungwa (Kulia) akimsikiliza kwa Makini Mkurugenzi Mkuu wa Kiwanda cha Nguo NIDA na NAMERA  (Picha zote na Amani Mbwaga)