Tuesday, July 16, 2019

Waziri Bashungwa Azindua ligi ya Mpira wa Miguu Karagwe


Na Amani Mbwaga,  Karagwe

Waziri wa Viwanda na Biashara ambae pia ni Mbunge wa Jimbo la Karagwe Mkoani Kagera Mhe. Innocent Bashungwa Mapema Wikendi iliyopita amezindua rasmi Mashindano ya ligi ya mpira wa miguu ambayo hufanyika kila mwaka Jimboni kwake na ni maarufu kwa BASHUNGWA KARAGWE CUP.

Akiongea na Wananchi katika kijiji cha Nyakagoyagoye Wilayani Karagwe wakati wa uzinduzi wa ligi hiyo Waziri Bashungwa amesema  wananchi wanapoendelea kuchapa kazi serikali nayo inaendelea kuleta huduma za jamii katika maeneo yote mijini na vijijini.

“Wana Karagwe Chapeni Kazi lakini sisi kwenye huduma za jamii suala la maji mlikuwa mkisikia nikiwa bungeni nazungumzia mradi wa maji mpaka koo linakauka, lakini huo mradi ndugu zangu ni mkubwa sana na uko katika hatua nzuri na hivi ninavyozungumza Waziri wa maji alikuwa hapa Karagwe jana kuhakikisha mradi huo unatekelezwa ipasavyo” alisema

Wakati huo huo Waziri Bashungwa amemshukuru Rais Magufuli kwa kupeleka miradi mingi na mikubwa Wilayani Karagwe ambapo hivi  karibuni tu Zaidi ya Bilioni 70 zitapelekwa tena katika Wilaya hiyo kwa ajili ya kuchochea miradi mingine ya maendeleo.

Mkuu wa Wilaya Karagwe Mhe. Godfrey Mhehuka amempongeza waziri Bashungwa kwa kuchapa kazi na hatimae wana karagwe wanafurahia maendeleo yanayopatikana ktokana na juhudi zake.
“Niemona niseme pongezi zangu kwako, umati huu ni mkubwa sana na unaona ni kwa sababu wewe umeamua kufanya kitu.

Aidha. Mhe Mheuka ameendelea kusema rais hakukosea kumchagua kuwa waziri wa viwanda na biashara hivyo amemuomba akachape kazi na wao wako nyuma yake kuhakikisha anawatumikia vyema wananchi wa Karagwe na Taifa kwa ujumla.

“Niseme neno moja tu, Mungu ametuona, nataka niwape siri hakika mungu amewaona DC Mwenye Waziri Mkoa wa Kagera niko peke yangu ahsanteni sana”alisema Mhe. Mheuka

Kwa mujibu wa mratibu wa mashindano ya BASHUNGWA KARAGWE CUP Bwana Majaliwa Said amesema  Mashindano hayo yameanza tarehe 13 Julai 2019 yakihusisha timu kutoka kata zote 23 za Halmashauri ya Wilaya Karagwe.

Jiogarafia ya karagwe ni kubwa hivyo tumetengeneza kanda mbalimbali ambazo zitakuwa  zinashindana na baadae kuingia katiak 16 bora hadi fainali
HABARI PICHA

Waziri wa Viwanda na Biashara Mhe.Innocent Bashungwa (Kushoto) akifurahia jambo na Mkuu wa Wilaya Karagwe Mhe.Godgrey Mhehuka katikati ni Katibu wa CCM wilaya ya Karagwe Bi. Mary Kananda
Pichani, Waziri wa Viwanda na Biashara Mhe. Innocent Bashungwa wa (tatu kushoto) akiwa pamoja na moja ya Timu iliyozindua mchezo wa kwanza wa ligi ya Bashungwa Karagwe Cup





Waamuzi na Ma Kapteni wa Timu

Baadhi ya Wananchi waliofika Kuhudhuria Uzinduzi wa Bashungwa Karagwe Cup Wkifuatilia kwa Makini Mchezo unaoendelea

Mratibu wa Mashindano ya BASHUNGWA KARAGWE CUP Bwana Majaliwa Said akitoa Taarifa ya Mashindano kwa Waziri wa Viwanda na Biashara  (Mbunge Karagwe) 



Wawakilishi wa Timu mbalimbali kutoka katika Kata 23 za Halmashauri ya Wilaya Karagwe wakifurahia Vifaa vya jezi na mipira vulivyotolewa na Waziri Bashungwa  wakati wa Uzinduzi wa Mashindano hayo. (Picha zote na Amani Mbwaga)

No comments:

Post a Comment