Tuesday, December 11, 2018

DC Mufindi, Serikali yaanzisha Kamandi ya Jeshi la Akiba


Na Amani Mbwaga, Mufindi
Hayo yamesemwa jana wakati wa hafla ya ufungaji wa mafunzo ya Jeshi la akiba  (Mgambo) yaliyofanyika katika kata ya Mninga Tarafa ya Kasanga wilayani Mufindi Mkoani Iringa ambapo mgeni rasmi wa hafla hiyo alikuwa ni Mkuu wa Wilaya na Mwenyekiti wa Kamati ya ulinzi na usalama  (W) Mufindi Mhe. Jamhuri William.

Katika hotuba yake Mhe William alisema mafunzo ya          Jeshi la akiba  ni mafunzo ambayo yako rasmi kabisa katika utendaji kazi wa serikali na yapo kwenye katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania  ya mwaka 1977.

Ndio maana kwa kutambua umuhimu wa Jeshi la akiba serikali imeanzisha maalumu Kamandi ya Jeshi la Akiba ambalo ni rasmi katika miongozo na usimamizi wa Jeshi la Ulinzi wa Wananchi JWTZ.

Kwa hiyo sio mafunzo ambayo ni lele mama, bali ni mafunzo ambayo yamezingatia sera kanuni, taratibu na miongozo yote inayohusiana na ulinzi wa Taifa la Tanzania.

“Vijana mimi kama mwenyekiti wa Kamati ya Ulinzi na usalama Wilaya Mufindi nawapongeza sana na nawatia shime endeleeni na uzalendo huo na Mungu atawabariki katika utumishi wenu” Alisema.
  
Serikali wilayani mufindi imedhamiria katika shughuli zote za kiserikali itawatumia askari hao wa Jeshi la Akiba pamoja na askari wengine katika shughuli zote za kitaifa.

“Hivyo natoa wito Makampuni mbalimbali yanayotaka kufanya kazi Mufindi na wanahitaji walinzi basi wasihangaike wala kuangalia pembeni wahakikishe wanachukua vijana hawa kwa sababu tayari wameiva na wana uzalendo mkubwa katika kulitumikia Taifa.

Akitoa taarifa ya mafunzo Mshauri wa Jeshi la Akiba  Wilaya Mufindi Meja RN Mwasakyene alisema mafunzo hayo yalianza tangu trehe 02 Julai 2018 wakiwa jumla ya wanafunzi 220, Wanawake  wakiwa idadi 45 na Wanaume idadi  175.

“Mpaka leo hii tunawahitimu 217 wanaume wakiwa idadi 173 na wanawake 44 sababu za wengine kushindwa kuendelea ni utovu wa nidhamu na hasa utoro wa muda mrefu” alisema Meja Mwasakyene.

Aidha masomo yaliyofundishwa ni utimamu wa mwili, ujanja wa porini, uhandisi, mbinu za kivita, usomaji wa ramani, mabomu ya mkono na baadhi ya silaha.

Akisoma Risala ya utii kwa mgeni rasmi mmoja wa wahitimu alisema walisoma pia masomo ya uraia ikiwemo  zimamoto , uhamiaji, kuzuia na kupambana  na rushwa  na hatimae usalama wa raia.

Vijana hao wakati wa mafunzo yao walishiriki pia katika kufanya huduma za kijamii ikiwemo kuchimba mshimo ya vyoo katika shule ya msingi Lugoda iliyopo kata ya Mninga.

Aidha wameomba mikataba ya ulinzi katika sekta binafsi au serikalini itolewe pale wanapopata fursa ya kuajiliwa wanataka wajue mikataba hiyo lakini pia na mkuu wa wilaya awe anaifahamu kwani ndio mtetezi wao mkuu, wanaamini atawasaidia.

Kwa upande wake Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya Mufindi na Diwani wa kata ya Mninga Mhe Fsto Mgina amewapongeza wahitimu hao wa Jeshi la akiba kwa kumaliza mafunzo yao salama na kusema wao kama viongozi wa serikali wanafarijika sana kuona vijana wanamaliza mafunzo hayo kwani watakuwa chachu ya maendeleo.

Baadhi ya wahitimu wa mafunzo hayo ya jeshi la akiba walipata wasaa wa kueleza furaha yao akiwemo Mhitimu Vivian Kihombo Msichana mashuhuri aliekuwa paredi kamanda amesema “Mimi nilichojifunza katika mfunzo haya ni kuwa mzalendo aidha nawahamasisha vijana wenzangu waje kufanya mafunzo haya na kamwe wasiogope”

Nae Mhitimu Zaire Januari Mdeta alisema “ Mimi nimepata faida ya kuwa timamu kimwili, na kiakili  lakini pia naipenda nchi yangu ndio maana nimjifunza uanajeshi ili niweze kutetea raia na mali zao na niko tayari hata kufa kwa ajili ya wengine kupona na kutetea taifa langu”.

Hafla hiyo iliambatana na maonesho ya gwaride, singe, kwaya na shairi.


HABARI PICHA
Mgeni Rasmi Mkuu wa Wilaya Mufindi Mhe Jamhuri William akipokea Salamu ya Heshima

Mgeni Rasmi Mkuu wa Wilaya Mufindi Mhe Jamhuri William Akitoa Hotuba


Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya Mufindi  na Diwani wa Kata ya Mninga Mhe.Festo Mgina akitoa salamu za kata yake.

Wahitimu wa mafunzo ya Jeshi la Akiba Mufindi


Mshauri wa Jeshi la Akiba Wilaya ya Mufindi Meja RN Mwasakyeni akitoa Taarifa ya Mafunzo
Paredi ikipita mbele ya Mgeni Rasmi kwa Mwendo wa pole Ikiongozwa na Paredi Kamana Vivian Kihombo 


Paredi ikipita mbele ya Mgeni Rasmi kwa mwendo wa Haraka





Msoma Risala akikabidhi kwa Mgeni Rasmi DC Mufindi


Kamati ya Ulinzi na Usalama Wilaya ya Mufindi
Kikundi cha Singe


Kikundi cha Kwaya



Pichani Mgeni Rasmi Mkuu wa Wilaya Mufindi (Katikati) akiwa na Kamati ya Ulinzi na Usalama Wilaya ya Mufindi

Mgeni Rasmi DC Mufindi Katikati akiwa na Wakufunzi wa Jeshi la Akiba Wilaya ya Mufindi

Mkuu wa Wilaya Mufindi Mhe Jamhuri William Katikati akiwa katika picha ya pamoja na Viongozi wa Paredi ya Wahitimu wa Jeshi la Akiba Mufindi

Mgeni Rasmi DC Mufindi akiwa katika Picha ya Pamoja na Washindi waliopewa zawadi kwa kufanya vizuri zaidi katika mafunzo yao






Ugeni ukiondoka kutoka Uwanjani (Picha zote na Amani Mbwaga)

No comments:

Post a Comment