Tuesday, August 21, 2018

Ziara ya Madiwani Kamati ya Fedha Uongozi na Mipango Halmashauri ya (W) Mufindi yakagua Miradi ya Maendeleo na Kuridhishwa nayo

Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya Mufindi Mhe Festo Mgina akipampu maji katika kisima kinachotumiwa na Wanafunzi wa Shule ya Sekondari Mgalo Kulia ni Makamu Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya Mufindi na Diwani Kata ya Sadani Mhe Ashery Mtono (Picha na Amani Mbwaga)
Na Amani Mbwaga, Mufindi
Ziara ya Waheshimiwa Madiwani Kamati ya Fedha Uongozi na Mipango Ikiongozwa na Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya Mufindi Mhe Festo Mgina Kukagua Miradi ya Maendeleo ikiwa ni Robo ya Nne 2017/2018

Kamati Imetembelea na Kukagua Miradi ya Ujenzi wa Madarasa 02 na Ukarabati wa Madarasa 04 katika Shule ya Sekondari Igombavanu.

Imetembelea na Kukagua Lambo la Maji lililojengwa kutokana na Juhudi za Wanufaika wa Mfuko wa TASAF Ambaposasa linatumika katika Shughuli za Kilimocha Umwagiliaji na Unyweshaji Mifugo katika Kata ya Igombavanu.

Aidha Kamati iikagua Mradi wa Ujenzi wa Hosteli ya Wasichana katika Shule ya  Sekondari ya Mgalo iliyopo kata ya Sadani ambayo Mpaka sasa imejengwa kwa nguvu za Wananchi na Mbunge wao.

HABARI PICHA
Kamati ya Fedha Uongozi na Mipango Ikikagua Madarasa yaliyokarabatiwa na Serikali  tayari kwa matumizi ya Wanafunzi Katika Shule ya Sekondari Igombavanu


Madarasa  04 ya Shule ya Sekondari Igombavanu yaliyokarabatiwa na Serikali
Madarasa Mapya 02 yaliyojengwa na Serikali katika Shule ya Sekondari Igombavanu

Ukaguzi wa Choo cha Wanafunzi Kikikiwemo cha Walemavu Shule ya Sekondari Igombavanu


Lambo la Maji Lililopatikana kutokana na Juhudi za TASAF Ktika Kusaidia Kaya Masikini amblo linatumika katika Kilimo cha Umwagiliaji na Kunyweshea Mifugo Katika Kata ya Igombavanu
Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya Mufindi Mwenyesuti akipokea Malezo ya Mradi kutoka kwa Mwenyekiti wa Kijiji cha Igombavanu Katikakti ni Mratibu wa TASAF na Mwisho ni Makamu Mwenyekiti Halmashauri ya Wilaya Mufindi

 
Mwenyekiti wa Kijiji cha Igombavanu aliyeinama chini akionesha shamba la Matikiti Maji Yanayolimwa  kutokana na Umwagiliaji wa Lambo la Maji


Afisa Mtendaji Kata ya Sadani (Kulia) Bwana Romanus Nyigo akitoa Taarifa ya Mradi wa Ujenzi wa Hosteli ya Shule ya Sekondari Mgalo Mbele ya Kamati ya Fedha na Mipango

Kamati Ikikagua Ujenzi wa Hosteli ya Wasichana Iliyojengwa kwa Nguvu za Wananchi Katika Shule ya Sekondari Mgalo


Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya Mufindi Mhe Festo Mgina akipampu maji katika kisima kinachotumiwa na Wanafunzi wa Shule ya Sekondari Mgalo Kulia kwake ni Afisa Elimu Sekondari Bwana John Lupenza


Picha zote na Amani Mbwaga

Mob:+255 656632566
E-mail:prof.mbwaga@gmail.com

No comments:

Post a Comment