Na Amani Mbwaga Mafinga.
Halmashauri ya
Wilaya Mufindi Imevuka lengo la Ukusanyaji Mapato yatokanayo na vyanzo vya
ndani katika mwaka wa fedha 2017/2018, na kufikia silimia 90.96.
Hayo yamesemwa na
Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya Mufindi Mhe Festo Mgina wakati wa kutano wa
Baraza la Madiwani la robo ya nne lililofanyika leo katika Ukumbi wa Halmashauri
ya Wilaya Mufindi Mkoani Iringa.
Ilielezwa kuwa
katika kipindi cha Julai 2017 hadi Juni 2018 Halmashauri ilikusanya na kupokea
jumla ya Tsh Bilioni 35.3 kati ya mapato hayo Tsh Bilioni 3.5 ni mapato yaliyotokana
na vyanzo vya ndani, Tsh Bilioni 24.6 ni mishahara, Tsh bilioni 5 ni miradi ya
maendeleo na Tsh Bilioni 2 ni matumizi ya kawaida.
Aidha katika kipindi
cha Julai 2017 hadi Juni 2018 mchango wa wananchi katika kutekeleza miradi ya
maendeleo ulikuwa na thamani ya Tsh Milioni 793.5.
Mlinganisho wa
mapato halisi ya Tsh Bilioni 35.3 kwa kipindi cha Julai 2017 hadi Juni 2018 na
makisio ya Tsh Bilioni 51.13 ya mwaka 2017/2018 unaonesha kuwa Halmashauri
imekusanya asilimia 68.4 ya lengo la mwaka wa fedha wa 2017/2018.
Aidha mlinganisho wa
mapato yatokanayo na vyanzo vya ndani yaliyokusanywa kwa kipindi cha Julai 2017
hadi Juni 2018 ya Tsh Bilioni 3.5 na
makisio ya mapato yanayotokana na vyanzo vya ndani ya Bilioni Tsh 3.8 kwa
kipindi hicho yanaonesha kuwa Halmashauri ya Wilaya Mufindi imekusanya asilimia
90.96 ya lengo la mwaka.
“Mimi nawapongeza
sana Mkurugenzi na timu yako kwa kufikia mafanikio Makubwa ya ukusanyaji mapato
katika Halmasahuri yetu, niwasihi muendelee kufanya vizuri zaidi katika
ukusanyaji lakini pia ni lazima tuongeze kasi na kuwa wabunifu wa kuwapata watu
wakorofi wanaokwepa kulipa ushuru na kodi mbalimbali za serikali”
alisema Mhe Mgina.
Aidha amewaasa
Waheshimiwa Madiwani kushirikiana na kuendelea kujenga Mahusiano mazuri zaidi na
Ofisi ya Mkurugenzi na wataalamu wake ili kuwaletea maendeleo wananchi wa
Mufindi na Taifa kwa ujumla.
Kwa upande wake Mkuu
wa Wilaya Mufindi Mhe Jamhuri David William aliwashukuru waheshimiwa madiwani kwa
kuasidia utekelezaji wa majukumu ya serikali na hasa katika uhamasishaji wa
kampeni ya ujenzi wa vyoo bora kwa wanachi.
Mhe Mwenyekiti tumezindua
kampeni ya ujenzi wa vyoo bora kwenye wilaya yetu na haya ni maelekezo ya
serikali, na sisi mufindi katika utekelezaji wa hilo tumejipa hadi tarehe 30
Oktoba 2018, tuhakikishe kila kaya inakuwa na choo bora. Alisema
Mhe William.
Tafsiri ya choo bora
tayari imekwishatolewa na wananchi wanaelewa, waheshimiwa madiwani wote wameombwa
kuzungumza lugha moja, ili kuhakikisha wananchi wote wanakuwa na vyoo bora.
Utekelezaji wa
kampeni hiyo unaambatana na usimamizi wa sheria ya mazingira.
Takribani asilimia
20% ya kaya ndio zenye vyoo bora Wilaya ya mufindi na asilimia 80% ni vyoo
ambavyo si bora, kaya nyingi zinatumia vyoo vya asili sasa ni wakati wa
kuhakikisha jamii inakuwa na vyoo bora.
Nae Kaimu Mkurugenzi
Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya Mufindi Bwana Isaya Mbenje amewakumbusha
waheshimiwa madiwani kuhusu kulinda mali za asili na mazingira kwa ujumla
kutokana Msimu wa kulimo unaokuja hivi karibuni ambapo watu wakati wa kuandaa
mashamba huchoma moto hovyo unaoathiri mazingira na maliasili zilizopo.
“Katika Wilaya yetu
tunatarajia msimu wa kilimo na tunaanza maandalizi ya mashamba kwa ajili ya
kilimo hivyo tunaenda kuwa na kampeni ya kuhakikisha wananchi wanapoenda
kusafisha mashamba yao wasichome na maeneo mengine”
alisema Bwana Mbenje.
![](https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEhHWVqv0dGZsaF0YoJhBIRFajub-b56xJikzWGUNgzU8d0QVowNWHhJI9jTycK_NiukoAHjtgYx1RH5y_CD2pbW_Q78n_cuQ42GBRzeZP9uK8uqxS2EsngnS2c_1y-PQ5IoVlW9-8JSb4I/s640/IMG_4707.JPG)
No comments:
Post a Comment