Friday, October 5, 2018

Waziri wa Ujenzi Mhandisi Kamwelwe Ataka Mabasi Kuendeshwa na Madereva Wenye Umri wa Zaidi ya Miaka 45.



Na Amani Mbwaga, Mafinga.
Waziri wa Wa Ujenzi Uchukuzi na Mawasiliano Isaack Kamwelwe
Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Mhandisi Isaack Kamlwelwe anataraji kupeleka bungeni  mswaada wa sheria ya Mabasi kuendeshwa na Madereva wasio chini ya umri wa miaka 45 na kuendelea ili kupunguza ajali nyingi zinazotokea na kupoteza maisha ya watanzania.

Ameyasema hayo leo wakati wa ziara yake ya kukagua maendeleo ya matengenezo ya barabara ya lami ya Mafinga hadi Igawa ambayo imekamilika kwa takribani asiimia 98 kwa kipande cha Mafinga –Nyigo na kuridhishwa na hatua hiyo iliyofikiwa, na kusisitiza mambo madogomadogo yaliyobakia yakamilke kwa wakati na ndani ya mkataba ikiwemo uwekaji wa alama za barabarani na kupaka rangi.

Lakini imegundulika kuwa kuna eneo karibu na barabara kuna mmomonyoko mkubwa wa udongo lakini tayari TANROADS wanalifanyia kazi na usanifu unaendelea kwa ajili ya utekelezaji.

“Lakini nisikitike sana mara baada ya barabara kukamiika ajali zimeanza kuongezeka na nimeambiwa kwamba ajali nyingi zinatokana na magari yanayobeba mafuta madereva mnajisahau sana barabara imekuwa nzuri mnapiga spidi zote tu, hapana ni lazima tuweke sheria kali, ndugu zangu tutembee taratibu kwa sababu tunakokwenda tutafika tu” alisema Mhe Kamwelwe.

Mhe Waziri ameleza kuwa miundo mbinu hiyo imeimarika ikiwa ni utekelezaji wa ilani ya chama tawala chama cha Mapinduzi waliahidi na wanatekeleza aidha utekeelezaji huo umefikiwa kwa sababu watu wamekubali kulipa kodi, Mhe Rais Dkt John Pombe Magufuli amesimama imara kuhakikisha kodi inarudi kwa wananchi ili waitumie ipasavyo.

“Uboreshaji mzuri wa barabara usigeuke kuwa vilio vya familia nasisitiza tutembee taratibu, baada ya kuona ajali zinakuwa nyingi mimi nitaomba wabunge mnikubalie inabidi tupeleke mswaada wa sheria bungeni dereva anae endesha basi ya abiria asiwe chini ya miaka 45 hatuna namna nyingine maana hatutaki kuona tunaendelea kuuwa ndugu zetu  watanzania kwa sababu ya mtu kuendesha gari akiwa na umri ambao haujafika miaka 45 na sisemi ndio nimeagiza sas hivi, hapana napeleka mswaada wa sheria bungeni  ili tuupitishe” alisema Mhe Waziri.

Hilo limekuja baada ya kufanya utafiti kutoka kwa Mhandisi Mshauri aliyekuwa akitafiti vyanzo vya ajali nyingi barabarani na kugundua kuwa kwa sehemu kubwa ajali nyingi zinasababishwa na Binadamu (Human Error) sasa ni lazima kuweka sheria mbalimbali ii kupunguza na kuondoa kabisa ajali.

Aidha Mhe Waziri alianza ziara yake iringa mjini na kukagua maendeeo ya marekebisho ya uwanja wa ndege iringa ambapo upo katika hatua za mwisho kukamilika na tayari kwa  kuanza kutumika.

“Nimeelekeza wakurugenzi waende kukagua na sina wasiwasi mwezi huu pengine kama watajiridhisha na masuala ya kiusalama kama yamekamilika basi ndege za shirika la ndege Tanzania zitaanza safari zake za Iringa” alisema Mhe Kamwelwe



HABARI PICHA
Barabara ya Mafinga - Igawa


Waziri waUjenzi Mhandisi Kamwelwe Kushoto akitata jambo na Mkuu wa Wilaya Mufindi Mhe Jamhuri William (kulia)

Waziri wa Ujenzi Mhandisi Kamwelwe akisalimiana na Mwenyekiti wa Halmashauri ya Mji Mafinga



Waziri wa Ujenzi Mhandisi Kamwelwe Akisalimiana na Mbunge wa Mafinga Mjini Mhe. Cosato Chumi




Eneo lenye mmomonyoka wa udongo linaloelekea kuhatarisha usalama wa barabara liko kama mita 30











Waziri Kamwelwe akisalimiana na Mbunge wa Mufindi Mhe Menrad Kigola

 


Waziri wa Ujenzi Uchukuzi na Mawasiliano Mhe Kamwelwe akiagana na Mwenyekiti wa CCM Wilaya ya Mufindi ndugu Yassin


Picha ya Pamoja
Picha zote na Amani Mbwaga

No comments:

Post a Comment