Tuesday, October 9, 2018

Waziri Jenista Mhagama Aongelea Mkakati wa Kuboresha Ajira kwa vijana kupitia mradi wa Kitalu Nyumba Kwa Kila Halmashauri.


Na Amanni Mbwaga, Mafinga.
Waziri  Jenista Mhagama akipokea zawadi ya Asali ya nyuki wasiouma 
Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu Sera, Bunge, Kazi, Vijana, Ajira na Walemavu Mhe Jenista Joakim Mhagama Ameongelea Mkakati wa Kuboresha Ajira kwa Vijana Kupitia Mradi wa Kitalu nyumba (Green House) Kwa Kila Halmashauri.

Ameyasema hayo alipofanya ziara yake katika Halmashauri za Wilaya ya Mufindi “tumefanya Utafiti tumeona kiwango cha upungufu wa ajira kinazidi kupungua, sasa hivi tumefikia kiwango cha asilimia 10.3” alisema Mhe Mhagama.

Serikali imefanya utafiti wa nguvu kazi iliyopo na kugundua asilimia 56 ya nguvu kazi yote ni vijana, na wengi wao waliomaliza darasa la saba na kidato cha nne hawana ujuzi kabisa hivyo kazi kubwa ya wizara ni kutoa mafunzo ya ujuzi kwa vijana ili watoke kwenye asilimia 79.9 angalau ifikie asilimia 54.
Mhe Mhagama ameziagiza Halmashauri kote nchini kutafuta vijana 100 watakaopata mafunzo kwa muda wote katika kitalu nyumba (Green house) na huu utakuwa mpango endelevu kwa kila mwaka ili kufikia vijana 500 kwa kila Halmashauri.
Kunatakiwa kuwe na kitalu nyumba  (Green House) 500 mpaka 1000 zinazomilikiwa na vijana katika kila halmashauri, ambapo kunakua na uhakika wa soko, uzalishaji ambao unatija kwa vijana ili kujenga uchumi na hatimae kuchangia pato la halmashauri na Taifa kwa ujumla.

“Mkoa wa Iringa ni moja kati ya Mikoa 7 tu ambayo tulitoa taarifa kwa mikoa yote Tanzania bara lakini ni mikoa 7 ndio iliyoweza kuonesha uthubutu wa utekelezaji ikiwemo mkoa wenu wa Iringa hivyo nina wapongeza sana” alisema Mhe Mhagama.

Wilaya zote ambazo ziko katika mkoa wa Iringa zitanufaika na miradi hiyo mikoa mingine ni Ruvuma, Mwanza, Kagera, Simiyu, Manyara, Lindi na baadae kufikia mikoa yote Tanzania bara.
Mhe Waziri amehakikisha kwamba mwezi huu wa 10 mwishoni ni lazima utekelezaji wa miradi hiyo uanze kuonekana.

Ukweli ni kwamba ifikapo tarehe 30 oktoba kama kuna Halmashauri haijatekeleza vigezo vilivyowekwa ambapo ni mkataba baina ya Ofisi ya Waziri Mkuu na Halmashauri, basi   mradi utahamishwa na kupelekwa halmashauri zingine za jirani ili ziwe na faida ya miradi miwili na kuendelea.

Kwa upande wake Mkuu wa Wilaya Mufindi Mhe Jamhuri William amemuhakakikishia Mhe Waziri kusimamia ipasavyo mradi huo katika halmashauri zake za wilaya ya mufindi ili zisije zikanyang’anywa miradi hiyo kwa kushindwa kufikia vigezo, na amewaagiza wakurugenzi wote kuhakikisha wanasimamia ukamilishaji wa vigezo ili miradi iwe endelevu na ameapa kama mradi utahama basi na mkurugenzi wa halmashauri hiyo ajiandae kufungasha vilago vyake.

HABARI PICHA
Waziri Jenista Mhagama akiwasili katika ofisi za Mkuu wa Wilaya Mufindi na Kupokelewa na Mwenyeji wake Mhe Jamhuri William ambae ndie Mkuu wa Wilaya hiyo


Waziri Jenista Mhagama akisalimiana na Mwenyekiti wa Ccm Wilaya ya Mufindi Ndugu Daud Yassin



Waziri Jenista Mhagama akisalimiana na Mwakilishi kutoka Ofisi ya Katibu Tawala (RAS) Mkoa wa Iringa



Waziri Jenista Mhagama akisalimiana na Afisa Uhamiaji wa Wilaya Mufindi
Waziri Jenista Mhagama akisalimiana na Kamanda wa Zimamoto Wilaya ya Mufindi


Waziri Jenista Mhagama akisalimiana na Afisa Usalama wa Taifa Wilaya ya Mufindi
Waziri Jenista Mhagama akisalimiana na Kaimu Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Mufindi Bwana Isaya Mbenje




Mkuu wa wilaya Mufindi Mhe Jamhuri William (Kulia) akitoa taarifa ya Wilaya ya Mufindi kwa Mhe Waziri Jenista Mhagama








Afisa Kilimo wilaya ya Mufindi Bwana Lubuva akitoa maelezo utekelezaji wa mradi wa Kitalu nyumba kwa waziri Jenista Mhagama





Waziri Jenista Mhagama akifurahia zawadi ya Asali ya nyuki wasiouma kutoka kwa wajasiriamali wadogo ambapo kwa niaba yao Mkuu wa Wilaya Mufindi alikabidhi zawadi hiyo



Waziri Jenista Mhagama tayari kuendelea na Safari yake Jijini Dodoma 
Picha zote na Amani Mbwaga
Kwa Maoni au Ushauri
Wasiliana nasi
Mob: +255 656 632 566
E-mail:prof.mbwaga@gmail.com

No comments:

Post a Comment