Monday, October 22, 2018

DC Mufindi Asisitiza Kudumisha Amani Nchini.


Na Amani Mbwaga, Mufindi
Mkuu wa Wilaya Mufindi Mhe Jamhuri David William ameyasema hayo jana Jumapili kwenye ibada na Waumini wa dini ya kikristo katika Kanisa la EAGT Jerusalemu Tempo liliopo Mafinga Mjini baada ya kupata mwaliko kwa ajili ya kuwatembelea wananchi wake na kuona maendeleo ya Ujenzi wa Kanisa.

“Ninashukuru sana Kuja kuwasalimia Wakristo wenzangu Mlinipokea na familia yangu viuri sana toka nahamia Wilaya hii mpaka sasa tumekuwa wenyeji, nawaomba sana muendelee kudumisha Amani iliyopo katika Mji wetu wa Mafinga na Taifa kwa ujumla” alisema Mhe William

Aidha ameliomba kanisa kuendelea kuwaombea viongozi wote wa serikali kuanzia Rais Dkt John Pombe Magufuli na Wasaidizi wake ili waliongoze vyema Taifa na kuwaletea maendeleo watanzania kwa lengo la kufikia Tanzania tunayoitaka.

“Mimi kila wakati ninapoona kanisa limefurika namna hii huwa ninafarijika sana kwa sababu ninajua uimara wa kanisa ndio usalama wa Wilaya yetu na Taifa kwa ujumla” Mhe William. 

Amewaomba Waumini kuendelea kuiunga mkono serikali ya awamu ya tano ili iendelee kuwaletea maendeleo katika shughuli mbalimbali ikiwemo kampeni za Usafi wa Mazingira, chanjo, ulinzi na usalama katika mitaa na mengine mengi.

Ametoa wito kwa wageni wanaohamia Mafinga mjini na Wilaya ya Mufindi Kwa Ujumla wawe makini na janga la ukimwi kwani Mkoa wa Iringa unashika nafasi ya pili kitaifa kwa maambukizi ikiwa na asilimia 11.2 ikiongozwa na Mkoa wa Njombe hivyo wanatakiwa kuchukua tahadhari na asingependa kuona mgeni anakuja hapa mzima haafu anarudi kwao anumwa.

Wakati huo huo Mhe William Amechangia Mifuko 10 ya sementi kwa ajili ya shughuli za ujenzi wa kanisa la kisasa unaoendelea kanisani hapo na kuwaahidi kushirikiana nao katika kuwapatia fursa za ujasiriamali kinamama wa kanisa hilo wanaojishughulisha na ujasiriamali katika shuguli mbalimbali za kuwaletea maendeleo.

Kwa upande wake Mchungaji Wailes Howa wa kanisa hilo la EAGT Jerusalemu Tempo Mafinga Mjini amemkaribisha mkuu wa Wilaya na kumuomba aendelee kushirikiana na kanisa kwa maendeleo ya Taifa.
Mchungaji Howa amesema tunapokuwa na viongozi wanaomcha mungu huwa tunabarikiwaasana cha msingi ni mtu kuwa uhusiano na mungu na ndilo ambalo linabariki mioyo ya watu.

Mimi ni miongoni mwa Wapenzi au Washabiki wa Mhe Rais Dkt John Pombe Magufuli nimempenda sana hasa katika utendaji wake wa kazi na kanisa ni shahidi huwa ninamzungumza sana hapa kanisani, tulikuwa tuanahitaji watu wa namna hii ambao wanaweza kututoa sehemu moja kwenda nyingine.

Si kwamba wengine waliopita hawakufanya chochote hapana kila mmoja ana cha kwake alichokifanya anaamini atakaekuja mwingine nae atatutoa mahali tuulipo na kutupeleka kwingine na anaaamini Mungu atatengeneza wepesi na kutuletea mtu ambae atatutoa hapana kutufikisha sehemu nyingine.

Katika Ibada hiyo Mchungaji Howa alimpatia zawadi ya Biblia Mhe Mkuu wa Wilaya pia Umoja wa Wanawake wa Kanisa hilo  walimpatia zawadi mke wake ikiwa ni moja ya kuonesha upendo mkubwa walionao kwa Mkuu huyo ambae anaiongoza wilaya ya Mufindi vyema na hasa kwa kuzingatia sheria taratibu, kanuni na hofu ya mungu.   






























No comments:

Post a Comment