Saturday, January 12, 2019

JKT Tanzania SC Ikiwa ugenini imelazimishwa sare ya bila kufungana dhidi ya Lipili FC


.
Na Amani Mbwaga, Iringa.
Timu ya Jeshi la Kujenga Taifa JKT Tanzania imelazimishwa sare ya bila kufungana na kugawana pointi moja moja dhidi ya Timu ya Lipuli FC ya Mkoani Iringa wakati wa mchezo wa Ligi Kuuu Tanzania bara uliyochezwa jana katika uwanja wa Samora uliopo Iringa Mjini.

Kwa mujibu wa ratiba ya ligi kuu Tanzania bara Mchezo huo ulitakiwa kuchezwa jana Ijumaa lakini uliahirishwa kutokana na mvua kubwa kunyesha hali iliyopelekea uwanja kujaa maji na hatimae mchezo kusogezwa mbele na kucheza leo hii.

Mchezo huo ulihudhuriwa na viongozi mbalimbali kutoka Jeshi la Kujenga Taifa makao makuu na vikosi vya JKT akiwemo Mkurugenzi wa Michezo JKT, Mkurugenzi wa Habari na Uhusiano JKT, Kamanda Kikosi  Mafinga JKT, Afisa Habari wa Timu hiyo na maofisa wengine wa Jeshi ikiwa ni kuwatia moyo wachezaji na kuongeza ari ya ushindi katika michezo yao ya Ligi kuu.

No comments:

Post a Comment